Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[227]

 

 

 

Sikukuu za Mungu na Jinsi Zinavyohusiana na Uumbaji

(Toleo La 3.0 19980101-19980424-20070718)

 

Jarida hili linaokusudia kuonyesha kuhusu Sikukuu zilizoamriwa na Mungu na Sabato na Miandamo ya Mwezi na jinsi zinavyohusiana, kipindi au mahali zinapotakiwa kufanyika muafaka, kwenye “juma la uumbaji” kwenye Kitabu cha Mwanzo. Jarida hili pia linatathmini uhusiano wake wa ndani kati ya Sikukuu na vipindi vyake vinavyotakiwa kuadhimishwa.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1998, 2007 Wade Cox, based on a 1997 paper by Alan Williams)

(Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Sikukuu za Mungu Jinsi Zinavyohusiana na Uumbaji



Uumbaji wa Dunia ni jambo la kuanzia na la msingi katika mpangilio wa Sikukuu za Mungu. Kwa mujibu wa muundo wa uumbaji, juma la uumbaji linaanzia siku ya kwanza ya juma (Jumapili) na linaenda hadi siku ya saba au siku ya Sabato (Jumamosi). Juma hili linaonyesha kuweka taswira ya miaka elfu saba (2Petro 3:8), ambako kwamba, Jumapili inawakilisha taswira ya miaka elfu moja.

Mwanzo 1:2-3 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji. 3 Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru

 

Ni muhimu kujua kwamba kwenye muundo huu juma linalotangulia linaonekana pia kuwa kama ni siku ya Kwanza ya mwezi wa Kwanza kwa mtazamo wa kimapokeo wa kawaida. Siku ya Kwanza iliyo muhimu ilipaswa kuwa ni ile siku ya Kwanza ya mwezi wa Kwanza na hivi ndivyo ilivyokubalika kwa ujumla. Kuna idadi ya mambo yanayokihusu kipindi hiki maalumu yenye maana ya moja kwa moja na uumbaji na lengo lake la kwanza halisia, ambalo ni uumbaji wa mwanadamu. Kwa hiyo hii hatimaye inahusiana na mwelekeo wa kwenda kwenye Sikukuu za kwanza na utakaso wa wanadamu.

 

Siku ya Kwanza ya mwezi wa Kwanza ilitumiwa pia na Mungu kuiukarabati tena dunia kipindi cha Nuhu, Musa na katika marejesho mapya yaliyotabiriwa kwenye Biblia (Mwanzo 8:13). Maangamizo ya Dunia yalitangulia kutoka mwaka uliotangulia siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili baada ya Safina kufungwa siku ya kumi. (sawa na Mwanzo 7:9-11). Tendo hili la kuwatenga na kuwaweka kando mbali wateule kwa namna inayoonyesha kiuashirio kwa Pasaka ya pili, kama tutakavyoona baadae.

 

Siku ya Kwanza ya Mwandamo wa Mwezi wa Kwanza wa Abibu tangu kuanza kwa mhakato wa kulitakasa Hekalu la Mungu. Ni ushuhuda unaaonekana pia kwenye imani na dini ya Kiyahudi kwa wazi kabisa kimwili. Ni kama ilivyosemwa na Kristo, na kwenye Ukristo, jambo hili lina taswira ashirifu ya Hekalu la Mungu ambalo limejengwa kwa mawe yaliyo hai na Hekalu hilo ndilo sisi (1Petro 2:5; 1Wakorintho 3:16; 6:19 sawa na jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [Sanctification of the Temple of God (No. 241)].

 

Kuelekea chini hadi aya ya 31:

Mwanzo 1:31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.

 

Mwanzo 2:1-3  Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote. 2 Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. 3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.

 

Neno lililotafsiriwa akapumzika (SHD 7673) lililotumiwa kwene Mwanzo 2:3 linamaanisha kusimama au kuacha [kuto exertion] au kusimama baada ya kumaliza; kupumzika.

 

Sabato ya Juma

Siku ya saba ya mwezi wa Kwanza ina maana mbalimbali zinazoiashiria, zinazohusiana na wokovu wa mwanadamu. Tunaona kwamba kwenye juma hili la kwanza, siku ya Saba ya mwezi wa Kwanza ilikuwa pia ni Sabato.

 

Juma (na Sabato) imeoorotheshwa na Sikukuu za Mungu kwenye Mambao ya Walawi 23:1-3. Hii inaonyesha uhusiano wa moja kwa moja ilionao na hizi Sikukuu.

Mambo ya Walawi 23:1-3 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 2 Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Sikukuu za Bwana, ambazo mtazipigia mbiu kuwa ni makusanyiko matakatifu; hizi ni sikukuu zangu. 3 Mtafanya kazi siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, kusanyiko takatifu; msifanye kazi ya namna yo yote; ni Sabato kwa Bwana katika makao yenu yote.

 

Mungu anasema kwamba siku ya Sabato ni ya mapuziko. Tunapaswa kufanya kazi kwa siku sita kama Mungu alivyofanya alipokuwa anaumba, na akapumzika siku ya saba.

 

Sabato, kama tunavyoambiwa, inatukumbusha mapumziko ya Mungu na mwisho wa juma la uumbaji. Andiko linaonyehwa kwamba Sabato inaonyesha taswira ya mapumziko ya Mungu na utimilifu wa mambo aliyoyaumba na kuyafanya.

Mwanzo 2:3 Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya. 

 

Kwenye Injili ya Yohana 5:17, Kristo anasema kwamba ueue na Baba bado wangali wanafanya kazi. Mapumziko haya ya Mungu ni ashirio ya mapumziko yajayo, kama yanavyoonyeshwa kwenye waraka kwa Waebrania.

Waebrania 4:1-4  Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa. 2 Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. 3 Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu: 4 Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote;

 

Kwa muhibu wa tulivyoona hapa tunagundua kwamba Israeli wa kimwili hawakuingia kwenye raha au pumziko la Mungu Aliye Hai na ndio ulikuwa Mpango wa Mungu kuwa na Israeli wa kiroho na kuwafanya waingie kwene raha iliyotajwa kwenye aya ya 8:

Waebrania 4:8-9 Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye. 9 Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu. 

 

Katika Waebrania sura ya 3 na 4, tunaona kwamba Sabato ilikuwa inaashiria ahadi iliyotolewa ya raha au mapumziko kwa Israeli kutokana na maadui zake wakati walipokuwa kwenye Nchi ya Ahadi. Hatahivyo, hawakuipata kamwe hiyo raha au mapumziko kwa ajili ya kuasi kwao (Israeli hawakuzitii amri za Mungu). Historia ya Biblia ya Waisraeli hawa wa kimwili tunapaswa kuitumia ili kujifunza masomo, na pia kwa ajili ya unabii wa Siku za Mwisho.

 

Warumi 15:4 Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.

 

1Wakorintho 10:11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani

 

Sabato ni ishara pia ya kutolewa kwa watu wa Mungu kutoka utumwani hhuko Misri.

Kumbukumbu la Torati 5:12-15 Ishike siku ya Sabato uitakase, kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru. 13 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 14 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala ng'ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako ye yote, wala mgeni aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile vile kama wewe. 15 Nawe utakumbuka ya kuwa wewe ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri, na ya kuwa Bwana, Mungu wako, alikutoa huko kwa mkono wenye nguvu, na mkono ulionyoshwa; kwa sababu hiyo Bwana, Mungu wako, alikuamuru uishike sabato.

 

Kwa hiyo, kuna muunganiko kati ya siku ya kwanza ya Mikate Isiyo na Chachu na Sabato ya siku ya saba ya juma la uumbaji, kama siku ya kwanza ya mikate Isiyo na Chachu ambayo inaashiria pia kutoka kwao utumwani Misri.

Kutoka 12:47-51 Na wafanye jambo hili mkutano wa Israeli wote. 48 Na mgeni atakapoketi pamoja nawe, na kupenda kumfanyia Bwana pasaka, waume wake wote na watahiriwe, ndipo hapo akaribie na kufanya pasaka; naye atakuwa mfano mmoja na mtu aliyezaliwa katika nchi; lakini mtu ye yote asiyetahiriwa asimle. 49 Sheria ni hiyo moja kwa mtu aliyezaliwa kwenu, na kwa mgeni akaaye kati yenu ugenini. 50 Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli wote; kama Bwana alivyowaagiza Musa na Haruni, ndivyo walivyofanya. 51 Ilikuwa siku ile ile moja, Bwana akawatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri kwa majeshi yao.

 

Kutoka na kuondoka Utumwani kulikoandikwa kwenye Kutoka 13:3-10:

Kutoka 13:3-10 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa. 4 Ninyi mwatoka leo katika mwezi wa Abibu. 5 Itakuwa hapo Bwana atakapowaleta mpaka nchi ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Wahivi, na Wayebusi, nchi hiyo aliyowaapia baba zako kwamba atakupa wewe, ni nchi imiminikayo maziwa na asali, ndipo mtakapoushika utumishi huu katika mwezi huu. 6 Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba, nayo siku ya saba itakuwa ni sikukuu ya Bwana. 7 Mikate isiyochachwa italiwa katika hizo siku saba; mkate uliotiwa chachu usionekane kwako, wala chachu isionekane kwako, ndani ya mipaka yako yote. 8 Nawe utamwambia mwanao siku hiyo, ukisema, Ni kwa sababu ya hayo Bwana aliyonifanyia hapo nilipotoka Misri. 9 Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya Bwana ipate kuwa kinywani mwako; kwani Bwana alikutoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo. 10 Kwa hiyo utaitunza amri hii kwa wakati wake mwaka baada ya mwaka.

 

Uhusiano kati ya Sabato na Pasaka hata hivyo, uko kwenye juma la pili la juma la mwezi wa Kwanza. Kabla hatujauangalia uhusiano uliopo kati ya Sabaso na Pasaka na Idi ya Mikate Isiyo na Chachu, tunapaswa kuliangalia juma la kwanza la mwezi wa Kwanza.  Siku ya Kwanza ya mwezi wa Kwanza ilikuwa ni ya Utakaso wa Hekalu, na utaratibu wa huduma za Hekalu lilitayarishwa kwa ajili ya Mpango wa wokovu kama ilivyoonyeshwa kwenye Pasaka. Siku ya Saba ya mwezi wa Kwanza ni siku ya Utakaso kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa Kupotoshwa na ni ya muhimu sana kwenye muundo wa mwisho wa Hekalu ambako siku hii imeamriwa kuadhimishwa kwa ajili ya Utakaso (Ezekilei 45:18-20).

Ezekieli 45:18-20 Bwana MUNGU asema hivi; Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga mume mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya nyumba, na juu ya pembe nne za daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya mtu aliye mjinga, ndivyo mtakavyoifanyia nyumba upatanisho.

 

Ndipo tunapoona hapa kuwa kuna dhabihu ya muhimu sana ya kulitakasa Hekalu au Nyumba ya Mungu, ili kuliwezesha lifanye kazi zake kwa huduma za kulitakasa taifa kwenye Pasaka. Kwa hiyo Pasaka inakuwa kwenye mchakato au awamu ya pili au wiki ya pili ya uumbaji. Kwa hiyo, kitendo cha kuutakasa Ulimwengu ulikoandikwa kwenye kitabu cha Mwanzo ulielekea kwenye tendo la kujitakasa kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa kupotoshwa ili wawe na sehemu na kuhesabiwa kwenye mchakato uliopo kwenye Mpango wa Mungu. Soma jarida la Utakaso kwa Ajili ya Dhambi za Kupotoshwa (Na. 291) [Sanctification of the Simple and Erroneous (No. 291)].

 

Juma la kwanza la utakaso linaonyesha kwamba siku ya Saba ya Mwezi wa Kwanza la shughuli za Uumbaji ilikuwa ni siku ya Sabato. Kwa hiyo wazo au dhana utakaso sio la kulifanyia haraka, bali ni njia pekee muhimu ya kulitakasa kusanyiko ni kwa njia ya haraka. Kwa hiyo, matendo ya Mungu kwa wateule yanawezesha kwenye uumbaji wote kamili kuchukua sehemu yake kwenye Pasaka. Sabato kwa kawaida ni kipindi cha sikukuu lakini kitendo cha kufunga saumu kwa kuzitubia dhambi zilizofanywa kwa kupotoshwa na kutokujua ni ukweli uliotiliwa chumvi.

 

Ni suala la kimzunguko wa kila mmoja aweze kuletwa kwenye Imani kutoka kwenye harakati za wateule wakiwa kama kundi la kiroho linaloonekana kwenye Pasaka. Ingekuwa haiwezekani kwa mtu kuingizwa Hekaluni la Mungu akiwa kama Jiwe lililo Hai kutoka kwenye maadhimisho ya Pasaka kama haikuwa rahisi kutokana na mchakato wa utakaso wa wana wa kiroho wa Mungu. Mchakato huu unaashiriwa kwa utakaso wa juma la kwanza la mwezi wa Kwanza katika siku za Kwanza na Saba za mwezi. Ishara hii inaonyeshwa kwa kutoa dhabihu ya kondoo mke kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa kutoshwa na imeelezewa vizuri kwenye Hesabu 15:27-29. Dhambi hii iliyofanywa pasipo kujua au kwa kupo hwa na uthibitisho kwamba zinafanywa kwa utoaji wa dhabihu unafanyika ulimwenguni kote.

Hesabu 15:27-29 Tena kama mtu mmoja akifanya dhambi pasipo kujua, ndipo atasongeza mbuzi mmoja mke wa mwaka wa kwanza kuwa sadaka ya dhambi. 28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya huyo mtu akosaye, atakapofanya dhambi pasipo kujua, mbele za Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake; naye atasemehewa. 29 Mtakuwa na sheria moja kwa huyo afanyaye neno lo lote pasipo kujua, kwa huyo aliyezaliwa kwenu kati ya wana wa Israeli, na kwa mgeni akaaye kati yao.

 

Dhabihu hii ya kondoo jike imetimizwa katika Kristo akiwa kama kichwa cha Kanisa. Dhabihu ambayo ni Kanisa iliwakilishwa na kondoo jike (ambaye ni Mtamba Mwekundu) ni mmoja ya dhabihu chache za wanyama wakike zilizowahi kutolewa. Kwa hiyo, utoaji wa dhabihu ulifanyika uwezekane na Kristo na Wana wa Mungu wakiwa ni Malaika na wateule katika siku ya kwanza ya juma la mwezi wa Kwanza.

 

Dhabihu ya Pasaka ilimaanisha na uumbaji wa vitu, ambaye hatimaye aliruhusiwa mteule aletwe Kanisani wachukue mahala pao kwenye mchakato endelevu wa dhabihu ulio kwenye Mpango wa Mungu.

 

Pasaka ilikuwa kwene juma la pili la mwezi wa Kwanza. Kabla hatujaangalia maana yake tutatathmini Mpango mzima.

 

Juma la uumbaji kama Mpango wa Wokovu

Tunaweza kuona kutokana na utaratibu huu utekelezaji kwetu katika siku za mwisho. Sabato ya juma inatokana na juma la uumbaji. Kwa hiyo tunaweza kutendea kazi muundo huu wote na kuona kwamba Mpango wa Mungu umeonyeshwa kwenye mchakato wa juma la uumbaji.

 

2Petro 3:8 inasema kwamba siku moja ni sawa na miaka elfu, na vivyohivyo miaka elfu ni sawa na siku moja.

2Petro 3:8 8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

 

Miaka elfu sita imewekwa kwa mwanadamu chini ya Malaika walioasi.

2Wakorintho 4:3-4 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.

 

Waefeso 6:12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

 

Miaka elfu moja imewekwa kwa ajili ya Siku ya Bwana chini ya Kristo na wateule wake (Ufunuo 20:4).

Ufunuo 20:4  Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu.

 

Kwa hiyo, juma lenye siku saba linaonyesha Mpango wa Mungu wa wokovu. hata kuna mwingiliano wa kimahusiano na mwezi na sikukuu kama zikiangukia kila mwezi, ambao unaonyesha marudio wa harakati au sughuli za Mungu, zilizoonyeshwa pia kwenye matumizi ya wiki kama zinavyoonekana kwenye kila sikukuu kwenye mwezi husika.

 

Tungeweza kuliona juma la uumbaji kama kipindi cha miaka elfu saba, lakini kimatendo ni Pasaka tunapenda kuijua mchakato wa harakati zilizotangulia. Juma lenyewe linalitangulia juma ambalo linaloangukia Pasaka, inayoashiria uumbaji wa Malaika au Viumbe wa mbinguni, ambao kimsigi ni uumbaji wa vitu vinavyoonekana na ni muhimu kwa utakaso wa viumbe tunavyoviona. Siku ya Saba ya mwezi wa Kwanza ni siku maalumu kwa utakaso wa |Viumbe wote na ndiyo maana hasa inayoongelewa kwenye Waebrania 2:11. Masihi alikusudiwa ama kulengwa kwa matendo yake kwenye juma la pili la kuutakasa ulimwengu wote, kwa namna zote mbili, yaani kimwili na kiroho. Utakaso wa siku ya Saba ni ishara ya utaratibu wa kiroho wa Malaika na wateule katika harakati kama zinavyohusiana na mambo ya kimwili. 

Waebrania 2:11  Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;

 

Kaliuawa siku ya Jumatano alasiri la juma tulijualo la uumbaji. Siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza ni mwisho wa juma la pili la mwezi Nisani lililoanzia siku ya nane ya mwezi. Kwa hiyo, siku ya tisa ilikuwa ni siku ya kwanza ya juma la pili la mchakato wa uumbaji. Kwa hiyo, dhabihu ya Pasaka inafanyika kwenye juma la pili, na kwa kweli inawakilisha mapumziko ya Sabato ya juma la pili, ambaye ni Kristo.

 

Mwaka halisia wa Pasaka, hata hivyo, ulikuwa siku ya Jumatano na ashirio hapa lina maana nyingine, ambao unaweza pia kumaanisha na juma la uumbaji. (Kwenye jambo hili tunaweza kuhitaji siku ya kwanza ya mwezi kuwa iliangukia siku ya Alhamisi. Tungeweza kujionea hilo kwa maana ya mfano ulioachwa.)

 

Siku ya kutolewa sadaka Kristo kwa hiyo inaweza kuwa ilitajwa kwamba ilikuwa mwishoni mwa siku ya kmilenia ya 4. Kama tutaichuklia hii kuwa ni siku ya 14 ya Nisan, basi alichaguliwa kabla ya siku ya kwanza ya juma (ambayo ni siku ya 10 ya Nisan) – kwa kuhesabu kuanzia nyuma tangu Jumatano ya siku ya 14, ndipo tunaipata siku ya 10, ambayo ilikuwa ni Sabato na siku iliyotangulia kuanza kwa juma la pili la uumbaji. Kwa hiyo Masihi alitangulia juma lililokuwepo, akachaguliwa na kuwekwa kando kiroho na kuwa pia kwenye uumbaji wa kiroho.

Kutoka 12:3-6 Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja;
4 na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo.

5 Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi.

6 Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.

 

1Petro 1:20 inaongelea mwonekano wa Masihi kwetu katikA Siku za Mwisho.

1Petro 1:20 Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu;

 

Siku ya kumi ya mwezi Nisan kwenye maelezo haya inatokea kuwa tu kwenye juma la pili kwenye mchakato wenyewe ulivyokuwa katika mwaka 30 BK ambao unaashiria kuwa ulipangwa au kukusudiwa mapema kabla ya Imani na wateule kabla hawajajitoa kwenye ulimwengu huu unaoonekana.

 

Kristo ndiye mwanzilishi na mwendelezaji, mlengwa wa wokovu wetu (Waebrania 5:9; 6:20; 12:2).

Waebrania 5:9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

 

Waebrania 6:20  alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki.

 

Waebrania 12:2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu

 

Tunajua pia kwamba ufufuko wa wote kutoka kwa wafu utatokea katika Siku ya Mwisho.

Yohana 6:40 Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

 

Yohana 6:44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.

 

Yohana 6:54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho 

 

Yohana 11:21-26 Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. 22 Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa. 23 Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka. 24 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho. 25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

 

Kutokana na Maandiko haya Matakatifu tunauona ufufuko utafanyika Siku ya Mwisho ambao una maana lengwa yake na Sikukuu ya mwezi wa Saba.

 

Juma lililotokea kifo cha Kristo katika mwaka wa 30 BK – ambalo kusulibiwa kwake kulifanyika siku ya Jumatano – linaonyesha mfano kivuli huu muhimu kama tunavyoutendea kazi kwenye juma la uumbaji.

 

Tunaona kwamba Hekalu linasafishwa siku ya Kwanza na utakaso unafanywa siku ya Saba yake. Katika juma la kusulibiwa kwake ndipo Kristo alisafisha Hekalu yeye mwenyewe kutoka siku ya kwanza ya juma au Jumapili, kuliko kufanya hivyo siku ya Kwanza ya mwezi kama ilivyotakiwa ifanyike kwenye Hekalu kwa mujibu wa Torati.

 

Kwa hiyo tunaona shinikizo kubwa kufanyika kwenye juma la kusulibiwa kwake likionyesha kuwa ni ishara ya Mpango wa Wokovu wa wanadamu na utaratibu uliodhahiri. Harakati hizi tena zinatanguliwa na kitendo chake cha usafishaji wa Hekalu katika siku ya Kwanza ya juma (Jumapili) kama Mungu alivyoifanya upya tena Dunia kwene milenia ya kwanza.

Mathayo 21:10-14 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu? 11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya. 12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa; 13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. 14 Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya 

 

Kristo alikufa siku ya Jumatano, kama ilivyoelezewa kwa kina kwenye jarida la Majira ya Kusulibiwa na Kufufuka (Na.  159) [Timing of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)]:

 

Ili afanane na Ishara ya nabii Yona, alishinda siku tatu usiku na mchana kwenye tumbo la Nchi (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Upya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)]. Ufufuko wake ilifanyika Siku ya Mwisho, Sabato ya juma.

Mathayo 28:1 Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi.

 

Mathayo 28:5-6 Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. 6 Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa.

 

(Angalia Sehemu ya Nyongeza ili upate kuelewa kikamilifu kuhusu mlolongo wa matukio yaliyotokea juma hili.)

 

Pia kumbuka kwamba uingiaji huu wa shangwe mjini Yerusalemu ulifanyika katika Sabato iliyopita au Jumamosi ya siku ya 10 (Mwanakondoo aliyechaguliwa hata kabla ya kuekwa kwa misingi ya dunia!).

 

Kulichukua hili kwenye mtazamo halisi wa juma la uumbaji ya siku kuwa ni taswira ya miaka elfu, tunaona kwamba Jumatano, Alhamisi, Ijumaa na Jumamosi ni Siku za Mwisho. Sabato ya Jumamosi ni taswira au kivuli cha “pumziko la millennia”. Siku hii ya Mwisho pia ni siku ya ufufuo, ambao pia umefanyika mwishoni mwa siku hii ya mapumziko.

 

Milolongo ya siku Saba katika Mpango wa Wokovu

Tunona kuwa kuna idadi ya milolongo ya siku ya saba kutoka kwenye tukio la kusafisha lililofanyika katika siku ya kwanza ya juma hadi kufikia Pasaka ya juma linalofuatia. Hii kwa hiyo ilifuatiwa na Idi ya Mikate Isiyo na Chachu, ambayo iansiku saba.

 

Sikukuu ya Mjuma au Pentekoste (hesabu ya siku hamsini) inafikia baada ya Sabato saba. Kuna aina tatu ya mavuno ambayo tunatakiwa au kuamriwa tukajihudhurishe mbele za Bwana.

 

Vipindi vihi vitatu vya mavuno ya Mungu tumeamriwa kukusanyika pamoja mbele za Mungu. Kila vuno moja linawakilisha mavuno ya kiroho ya Mungu kwenye Mpango wa Wokovu (soma Kumbukumbu la Torati 16:16-17).

Kumbukumbu la Torati 16:16-17 Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu. 17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa. 

 

Pasaka/Mikate Isiyo na Chachu: majira ya kwanza ya mavuno

Sasa tutajoea kuhusu Idi ya Mikae Isiyo na Chachu kwa mtazamo au mlinganisho wa mavuno makuu matatu ya Mungu. Mavuno haya yanashabihiana na Krisro, Kanisa na ufufuo wa pumziko la wanadamu litakalofanyika mwishoni.

1Wakorintho 15:22-25 Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. 23 Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja. 24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. 25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

 

Maadhimiso ya Mikate isiyo na Chachu ni majira ya mavuno ya kwanza au malimbuko kati ya matatu. Pentekoste ni ya Pili na Vibanda ni ya tatu (Kutoka 34:18-23). Kwa hiyo, inafuatiwa kwamba majira haya ya mavuno ya kwanza yanaashiria taswira ya majira ya kwanza ya Kristo – ambaye ni wa kwanza katik ya malimbuko ya mavuno ya shayiri.

 

Tutaiangalia idi ya Mikate Isiyo na Chachu kwa mtazamo wa taswira yake kwa majukumu au kazi za Kristo katika wokovu wa wanadamu.

 

Juma la Mikate Isiyo na Chachu kadhalika linamuonyesha Kristo aliyeuachinjwa kabla ya kuanza kwa siku ya kwanza.

Kutoka 12:6 Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.

 

Kuna matukio muhimu nay a maana matatu yanayoonyeshwa au kuilengwa kwenye siku za Mikate Isiyo na Chachu. Siku ya kwanza inaonyesha utimilifu wa kazi ya Kristo akiwa kama dhabihu safi isiyo na dhambi na ni Kuhani Mkuu aliyekuwa anajiandaa kuingia katika Patgakatifu pa Patakatifu mara moja tu kwa ajili ya wote na kwa damu yake mwe nyewe na sio ya mafahali ya ng’omba. Mganda wa Kutikiswa unaonyesha ukubalifu wa Mungu wa dhabihu ya Kristo na Kristo anapokea mamlaka yake ya kutawala amoja na ukuhani mpya.

Danieli 7:13-14 Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. 14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.

 

Ufunuo 1:6 na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina.

 

Siku ya mwisho ya Mikate Isiyo na Chachu inaashiria kazi ya Kristo katika Siku za Mwisho akiwa kama Mfalme.

 

Kama tutalilinganisha juma la Mikate Isiyo na Chachu na juma lenyewe lilivyokuwa mwaka 30 BK, siku ya kwanza inaionyesha kazi ya Kristo kwenye juma la uumbaji (Waebrania 1:2). Mganda wa Kutikiswa unaonyesha jukumu la Kristo kama mwokozi aliyekubaliwa na Kuhani Mkuu aliyechaguliwa na Mungu katika siku ya nne (Jumapili ya Mganda wa Kutikiswa), inayotokea kwenye Jumatano ya juma la uumbaji, na kwa hiyo ni siku ya mwisho ya Mikate Isiyo na Chachu ambayo pia ni mapumziko.

 

Siku ya mwisho ni Sabato kwa kuwa kazi ya Kristo katika kipindi cha Milenia (au mwaka wa elfu moja wa “juma la uumbaji”, Sabato). Hii ni kazi yake itakavyokuwa katika Siku ya Bwana. Anakuja kama Mfalme katika Ujio wake wa pili wakati dunia itakapopata pumziko.

 

Siku hizi saba zinajulikana kwa tendo la kuondoa chachu ambayo inaonysha uondoaji wa dhambi maishani mwetu. Kristo aliishi maisha yasiyo na dhambi. Akiwa ni dhabihu isiyo na dhambi aliweza kupigilia tangazo la msamaha wa madeni au chierographon kwenye stauros au mtini. Kutokana na tukio hili, basi tumeokolewa.

 

Mkate Usio na Chachu unaonyesha ukombozi wetu kutoka dhambini, kama inavyoonyesha Kutoka 13:3-9, na tendo hili la kuiondoa dhambi ni endelevu kutoka maishani mwetu. Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu ina kiwango kingine cha kwanza cha maana ikiwa kama mavuno ya kwanza ya Mungu. Mkate Usio na Chachu ni majira ya mavuno ya ya Kristo. Haimaanishi mavuno ya Kanisa bali zaidi sana inaonyesha harakati za Kristo kwa kipindi chote na matayarisho ya Kanisa kwa mavuno yake. Na kwa hiyo kimuundo inatofautiana na Sikukuu ya Vibanda ambayo kwamba siku ya nane na siyo ya saba inakuwa ni Siku Takatifu, ambavyo siku hii ya mwisho inaonyesha au inalenga hitimisho la mpango aliouweka Mungu baada ya Milenia. Kwa hiyo, siku ya mwisho ya siku hizi saba za Vibanda sio Siku Takatifu.

 

Kuna mzunguko ndani ya wateule kuanzia utakaso wa Watakatifu hadi kipindi cha maadhimisho ya Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu, ambacho kinatumiwa kwa kuongoa chachu na hamira kwa wale walioitwa na kuchagulia tangu mwanzo ili kuwaandaa kumpokea Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste. Siku hamsini zinaashiria maisha yao tangia ukubwa wao tangu wakiwa na umri wa miaka ishirini. Wanapoongoka, wanachukua mahala pao kwenye Utakaso wa kiroho wakiwa kama Wana wa Mungu ili wafundishe na kulitakasa kundi linguine la wale walioitwa watoke kwa Mpango wa Mungu.

 

Pentekoste au Idi ya Majuma: majira ya mavuno ya pili

Kuna Sabato saba za juma kuhesabiwa tangu siku ya Mganda wa Kutikiswa, na siku moja baada ya Sre are seven weekly Sabbathabato ya saba ambapo kunaadhimishwa Pentekoste. Mauma saba kyelekea Pentekoste yana idadi kadhaa ya matukio na mambo ya kuyatenda.

 

Yanaweza kuonekana kama ni zama ya saba ya Kanisa inayoelekea kwenye pumziko lijalo kwa mtindo endelevu.

Waebrania 4:3 Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu:

 

Waebrania 4:10  Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake

 

Inaweza pia kuonekana kuhusiana na kipindi cha Yubile, kama tuonavyo hapo chini.

 

Tendo la kuhesabu linaanzia tangu siku ya Mganda wa Kutikiswa. Kuelekea hadi P entekoste ni moja ya uchaguzi na kuachana na ukuhani mpya ulio chini ya Kuhani Mkuu aliye mfano wa Melkizedeki (sawa na Waebrania 5:6 to 7:21).

Waebrania 6:20 …mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki

 

Mganda wa Kutikiswa unaashiria kupaa kwa Kristo na ndenda kwenye chumba chenye Kiti cha Enzi cha Mungu ili akubalike baada ya kufufuka kwake toka kwa wafu, kama inavyoonekana kwenye Danieli 7:13-14 na Yohana 20:17.

Yohana 20:17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.

 

Kuna miaka saba ya Sabato, na hatimaye, mwaka unaofuatia baada ya huu wa saba wa Sabato, unakuwa ni mwaka wa Yubile. Kwa hiyo, kuna uhusiano kati ya Pentekoste na mwaka wa Yubile na huku miundo yote miwili ikiwa ni sawa. Muundo wa Yubile pia unaakisi maisha ya mtu mkamilifu aliye na miaka hamsini tangia utuuzima wake hadi kwenye umri wa miaka sabini na “mapumziko” yale yanatokutikana kwa Mungu. Waisraeli walizishika Pentekoste arobaini jangwani, ambayo pia inaonyesha upana wa matukio ya Mungu kwa Masihi. Kuna mambo ya kujifunza sisi. Sisi nasi tupo “jangwani” kwa kipindi cha Yubile arobaini (miaka 2,000) au Siku za Mwisho (Alhamisi na Ijumaa ya juma la uumbaji). Pentekoste inaakisi kuwa kwetu sisi malimbuko au matunda yavunwayo kwanza na kuwa kwetu “tuliomwagiliwa na kurutubishwa kwa maji” au kuongozwa na Roho Mtakatifu.

Yeremia 5:24  Wala hawasemi mioyoni mwao, Basi, na tumche Bwana, Mungu wetu, aletaye mvua, mvua ya mwaka, na mvua ya vuli, kwa wakati wake; na kutuwekea juma za mavuno zilizoamriwa.

 

Majuma yaliyowekwa ya mavuno kama yalivyoelezewa hapa ni majuma saba ya Pentekoste. Kwahiyo, kipindi cha Mganda wa Kutikiswa hadi Pentekoste kimetengwa na watu wa Mungu.

 

Pentekoste ni mavuno ya pili ya Mungu na wakati mwingine inatajwa kama ni Sikukuu ya Mavuno kama kwenye Kutoka 23:16 inavyoonyeshwa.

Kutoka 23:16 tena, sikukuu ya mavuno, hayo malimbuko ya kazi zako za kupanda mashambani; tena, sikukuu ya kukusanya, mwisho wa mwaka, hapo utakapokusanya hayo uliyoyataabikia shambani.

 

Inaonyesha mavuno endelevu ya kiroho na kuhukumiwa kwetu kwa kiwango endelevu pia (mikate ya kutikiswa). Inaitwa mavuno ya malimuko, kwa hiyo kuonyesha kuwa ni mavuno ya mwisho. Mikate ya kutikiswa siku ya Pentekoste inatiwa chachu.

 

Chachu ya kale ya uovu na dhambi inawekwa kwenye chachu mpya ya Roho Mtakatifu anayefanya kazi kwenye mambo mawili ya Kristo na kwenye Agano la Mungu. Maisha yetu yanamchanganyiko wa dhambi, lakini hatupo kwenye utumwa tena. Sadaka inayotolewa siku ya Pentekoste inaonyesha hitaji kwa ajili ya dhabihu ya dhambi ambayo ilitolewa kwa ajili yetu kupitia kwa Yesu Kristo ambaye aliitoa dhabihu ile mara moja tu na kwa ajili ya wote kwenye Pasaka. Kwa hiyo, tunatarajia mavuno yetu kwenye Pentekoste iwezekane kwa mavuno ya Kristo kwenye Pasaka. Sadaka ya dhambi inaashiria ondoleo la dhambi katika maisha yetu kwa kiwango endelevu (sawa na jarida la Chachu ya Kale na Mpya (NA. 106a) [The Old and the New Leaven (No. 106a)].

Mambo ya Walawi 23:15-21 Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba; 16 hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya. 17 Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba, itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa Bwana. 18 Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza wana-kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng'ombe mume mmoja, na kondoo waume wawili; watakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, pamoja na sadaka yao ya unga, na sadaka zao za kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza iliyosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto. 19 Nanyi mtasongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana-kondoo wawili waume wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani. 20 Kisha kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Bwana, pamoja na wale wana-kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa Bwana, wawe wa huyo kuhani. 21 Nanyi mtapiga mbiu siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yo yote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu' 

 

Kumbuka kuwa kuna mbuzi wa dhabihu ya dhambi anayeonyeshwa kwenye aya ya 19. Pia kumbuka kwamba Mganda wa Kutikiswa hauhusiani na matoleo ya sadaka ya dhambi, kwa kuwa unaashiria taswira ya Kristo aliyeishi maisha yasiyo na dhambi.

Mambo ya Walawi 23:9-14 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 10 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Hapo mtakapokuwa mmekwisha ingia hiyo nchi niwapayo, na kuyavuna mavuno yake, ndipo mtakapomletea kuhani mganda wa malimbuko ya mavuno yenu; 11 naye atautikisa mganda mbele za Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa. 12 Na siku hiyo mtakayoutikisa mganda, mtamsongeza mwana-kondoo wa kiume mkamilifu wa mwaka wa kwanza awe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana. 13 Na sadaka yake ya unga itakuwa sehemu za kumi mbili za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, ni kafara iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto kuwa harufu ya kupendeza; na sadaka yake ya kinywaji itakuwa ni divai, robo ya hini. 14 Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote

 

Tukiwa kama waumini tuliobatizwa katika mwili wa Yesu Kristo, tunahukumiwa kwa yale tunayoyatenda.

Ayubu 34:21-23 Kwani macho yake ya juu ya njia za mtu, Naye huiona miendo yake yote. 22 Hapana weusi, wala hilo giza tupu, Wawezapo kujificha watendao udhalimu. 23 Kwani yeye hana haja ya kumfikiria mtu zaidi, ili aende mbele za Mungu ahukumiwe.

 

Pentekoste inaashiria hii kuwa ni mikate ya kutikiswa, ambayo kwa matendo Israeli waliishika mata arobaini walipokuwa wakitangatanga jangwani. Kwa kuiunganisha hii kwenye Yubile kama ilivyosemwa kabla inaonyesha hukumu yetu kwa Mungu kwa msingi endelevu kwa kipindi cha miaka elfu mbili. Na mtume Petro alikuwa na la kusema kama hivi.

1Petro 4:17  Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?

 

Pentekoste ya kwanza ya Waisraeli ilikuwa wakati walipoipokea Torati pale Sinai. Pentekoste ya kwanza ya Kanisa la Agano Jipya ilikuwa wakati walipopokea Sheris iliyoandikwa ndani ya mioyo yao, kumwagiwa kwao na Roho wa Mungu.

 

Waebrania 8:10 10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.

 

Matendo 2:17-21 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. 18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri. 19 Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. 20 Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri. 21 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.

 

Kwenye Matendo 2:18 inasama “siku” (katika uwingi) na kwenye aya ya 17 inataja kuwa Siku za Bwana. Aya ya 20 inaweka siku hizi kabla ya siku ya mwisho: “... siku iliyo kuu na ya kuogofya ya Bwana”. Kwa hiyo, tunaziona siku mbili (Alhamisi na Ijumaa ya juma la uumbaji) au miaka elfu mbili hadi kufikia Milenia. Dhana nzima kuhusu Siku za Bwana imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192) [The Day of the Lord and the Last Days (No. 192)].

 

Kuna Sabato saba kamili tangu Mganda wa Kutikiswa (Kristo) hadi kwenye mavuno (Pentekoste) ya wateule. Pia inaeleweka kwamba kuwepo kwa zama ya Makanisa la saba kuliashiriwa na Makanisa saba ya Ufunuo sura za 2 na 3, na yanapaswa kukamilika kabla ya mavuno.

 

Maana ya baragumu

Baragumu au Tarumbeta zilitumika katika kuwaonya Israeli wakati wa vita. Zilipigwa pia kwenye Sikukuu, Miandamo ya Mwezi na wakati wa kutoa sadaka ya kuteketezwa na walipokuwa wanatoza sadaka za amani. Zilitumika kwa kupigwa ili kuwakusanya viongozi au watu pamoja na kuwapa maelekezo ya jinsi watakavyoondoka na kusafiri Israeli walipokuwa jangwani.

Hesabu 10:2-10 Jifanyie tarumbeta mbili za fedha; utazifanya za kazi ya ufuzi; nawe utazitumia kwa kuwaita mkutano wakutane, na kwa kusafiri kwao yale makambi. 3 Na hapo watakapozipiga hizo tarumbeta, mkutano wote utakukutanikia wewe, hapo mlangoni pa hema ya kukutania. 4 Nao wakipiga tarumbeta moja tu ndipo wakuu, walio vichwa vya maelfu ya Israeli, watakukutanikia wewe 5 Tena hapo mtakapopiga sauti ya kugutusha sana, marago yaliyoko upande wa mashariki yatasafiri. Tena hapo mtakapopiga sauti ya kugutusha ya pili, marago yaliyoko upande wa kusini watasafiri; 6 watapiga sauti ya kugutusha kwa ajili ya safari zao. 7 Lakini mkutano utakapokutanishwa pamoja mtapiga, lakini hamtapiga sauti ya kugutusha. 8 Wana wa Haruni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta; nazo zitakuwa kwenu ni amri ya milele katika vizazi vyenu vyote. 9 Tena hapo mtakapokwenda kupiga vita katika nchi yenu, kupigana na adui awaoneaye ninyi, ndipo mtakapopiga sauti ya kugutusha kwa tarumbeta; nanyi mtakumbukwa mbele za Bwana, Mungu wenu, nanyi mtaokolewa na adui zenu. 10 Tena katika siku ya furaha yenu, na katika sikukuu zenu zilizoamriwa, na katika kuandama miezi kwenu, mtapiga hizo tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa, na juu ya dhabihu za sadaka zenu za amani; nazo zitakuwa kwenu ni ukumbusho mbele za Mungu wenu; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

 

Hapa kulikuwa na baragumu mbili. Baragumu iliyopigwa kwa mlio mtulivu ilipigwa kuwaita na kukusanya viongozi. Ya pili ilitumika kuwaita na kuwakusanya wote. Baragumu zikipigwa kwa milio ya uwingi zinahusiana na kuwaita wateule na kwa taifa.

 

Kitabu cha Ufunuo kinatuambia kuna baragumu saba. Baragumu saba zina  mihuri wa saba. Mhuri unahusiana na sehemu ya gombo la maandiko, kwenye baragumu hizi ni ufunuo. Baragumu ya saba inafanya kurudi kwa Kristo akiwa kama Mfalme na kusanyiko la wateule. Baragumu ya saba inafunuka na kuwa kitasa cha saba cha ghadhabu ya Mungu. Kwa hiyo, Siku ya Baragumu inaashiria kipindi fulani na sio ni tukio tu. Tunapotazama kuhusu kutwaliwa kwa Yeriko, Kitabu cha Yoshua kinaonyesha ashirio la jambo hili pia. Waliuzunguka mji mara moja na kupiga baragumu kila siku kwa siku sita na katika siku ya saba walitembea wakiuzunguka mji mara saba na wakapiga baragumu kila mzunguko mmoja. Kisha, wakati walipokuwa wanazipiga baragumu mara ya saba na huku wakuzunguka, watu walipiga kelele kwa nguvu.

Yoshua 6:1-20 Basi Yeriko ulikuwa umefungwa kabisa kwa sababu ya wana wa Israeli; hapana mtu aliyetoka wala hapana mtu aliyeingia. 2 Bwana akamwambia Yoshua, Tazama, nimeutia Yeriko katika mkono wako, na mfalme wake, na mashujaa wake. 3 Nanyi mtauzunguka mji huu, watu wote wa vita, mkiuzunguka mji mara moja. Fanya hivi siku sita. 4 Na makuhani saba watachukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume, mbele ya hilo sanduku; na siku ya saba mtauzunguka mji mara saba, nao makuhani watapiga tarumbeta zao. 5 Kisha itakuwa watakapopiga hizo pembe za kondoo waume kwa nguvu, nanyi mtakaposikia sauti ya tarumbeta, watu wote watapiga kelele kwa sauti kuu; na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale, na hao watu watapanda, kila mtu akiendelea mbele kukabili. 6 Bali Yoshua, mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia, Lichukueni sanduku la agano, tena makuhani saba na wachukue tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Bwana. 7 Naye akawaambia watu, Piteni mbele, mkauzunguke mji, na hao watu wenye silaha na watangulie mbele ya sanduku la Bwana. 8 Basi ikawa Yoshua alipokwisha kusema na watu, wale makuhani saba, wenye kuzichukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele za Bwana, wakatangulia, wakazipiga hizo tarumbeta; nalo sanduku la agano la Bwana likawafuata. 9 Wale watu wenye silaha walikwenda mbele ya hao makuhani waliozipiga tarumbeta, na wale waliokuwa nyuma wakalifuata hilo sanduku; makuhani wakizipiga tarumbeta walipokuwa wakienda. 10 Yoshua akawaamuru watu, akasema Msipige kelele, wala sauti zenu zisisikiwe, wala neno lo lote lisitoke kinywani mwenu, hata siku ile nitakapowaamuru kupiga kelele, ndipo mtakapopiga kelele. 11 Basi akalipeleka sanduku la Bwana liuzunguke huo mji, likauzunguka mara moja, kisha wakaenda kambini wakakaa kambini. 12 Yoshua akaondoka asubuhi na mapema, nao makuhani wakalichukua sanduku la Bwana.13 Na wale makuhani saba wakazichukua tarumbeta saba za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Bwana, wakaendelea wakazipiga tarumbeta; nao watu wenye silaha wakawatangulia, na hao waliokuwa nyuma wakalifuata sanduku la Bwana; makuhani wakizipiga tarumbeta walipokuwa wakienda. 14 Siku ya pili wakauzunguka mji mara moja, wakarejea kambini; ndivyo walivyofanya siku sita. 15 Ikawa siku ya saba wakaondoka asubuhi na mapema wakati wa mapambazuko, wakauzunguka mji vivyo hivyo mara saba; ila siku hiyo waliuzunguka huo mji mara saba. 16 Hata mara ya saba makuhani walipozipiga tarumbeta, Yoshua akawaambia watu, Pigeni kelele; kwa maana Bwana amewapeni mji huu. 17 Na mji huu utakuwa wakfu kwa Bwana, mji wenyewe na vitu vyote vilivyomo; isipokuwa Rahabu, yule kahaba, ataishi, yeye na watu wote walio pamoja naye nyumbani, kwa sababu aliwaficha hao wapelelezi tuliowatuma. 18 Na ninyi, msikose kujiepusha na kitu kilichowekwa wakfu; msije mkakitwaa kitu kilichowekwa wakfu, baada ya kukiweka wakfu; nanyi hivyo mtayafanya matuo ya Israeli kuwa yamelaaniwa na kuyafadhaisha.19 Lakini fedha yote, na dhahabu, na vyombo vya shaba, na chuma, ni vitakatifu kwa Bwana; vitaletwa katika hazina ya Bwana. 20 Basi watu wakapiga kelele, na makuhani wakazipiga tarumbeta; hata ikawa, hapo watu waliposikia sauti ya tarumbeta hao watu wakapiga kelele kwa sauti kuu sana, na ule ukuta wa mji ukaanguka nchi kabisa, hata watu wakapanda juu, wakaingia katika mji, kila mtu akiendelea kukabili mbele; wakautwaa huo mji.

 

Kuna uhusiano wa wazi hapa kwenye upigaji wa baragumu ya saba ya Ufunuo 11:15,18 na katika baragumu au parapanda ya mwisho na upigaji wa Malaika Mkuu.

1Wathesalonike 4:16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

 

1Wakorintho 15:51-52 Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, 52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

 

Baragumu zilipigwa kwa siku saba zote za kipindi cha kuizunguka Yeriko. Tena tunaweza kuhusianisha hii hadi nyuma kwenye juma la uumbaji. Katika kutumia mlinganisho huu, ndipo tunauona mzingito wa Yeriko ukionyesha Mpango wa Mungu wa ukombozi ya sayari hii na maonyo kupitia kipindi cha miaka elfu. Sikm ya saba ni ashirio la kuja au kurudi kwa Masihi na kukomeshwa au kuangamizwa kwa Dunia hii na mifumo yhake yote. Masihi atafanya hivi kipindi atakapokuja mwanzoni mwa Milenia. Hii inahusianishwa na ujio wa Kiumbe wa aina ya malaika mtakatifu mapema katika siku ya saba ya mzingiro wa mji wa Yeriko. Ikumbukwe kwamba Kristo anaonekana kuwa alikuwepo akiwa kama Jemadari wa jeshi la BWANA”.

Yoshua 5:13-14 13 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? 14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake?

 

Kumbuka na kujua kwamba Kristo amekwisha kuja (aya ya 14). Pia kumbuka kuwa kitendo cha kumuokoa na kumlinda Rahabu wakati huu, alilindwa na kunusurika kwa ajili ya kamba nyukundu aliyoiweka dirishani kwake.

Yoshua 2:14-18 Wale wanaume wakamwambia, Uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa ihisani na uaminifu. 15 Ndipo akawashusha kwa kamba dirishani, maana nyumba yake ilikuwa katika ukuta wa mji; naye alikaa ukutani. 16 Akawaambia, Enendeni zenu mlimani, wale wanaowafuatia wasije wakawapata; mkajifiche huko siku tatu hata wao wanaowafuatia watakaporudi; kisha enendeni zenu. 17 Wale wanaume wakamwambia, Sisi tunataka tusiwe na hatia kwa ajili ya kiapo hiki ulichotuapisha. 18 Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotutelemshia; nawe uwakusanye kwako nyumbani mwako, baba yako, na mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako.

 

Yoshua 6:23-25 Basi wale vijana wapelelezi wakaingia, wakamtoa Rahabu, na baba yake, na mama yake, na ndugu zake, na vitu vyote walivyokuwa navyo, wakawatoa na jamaa zake wote pia; wakawaweka nje ya matuo ya Israeli.
24 Kisha wakauteketeza mji kwa moto, na vitu vyote vilivyokuwa ndani yake; bali fedha, na dhahabu, na vyombo vya shaba, na vya chuma, wakavitia katika hazina ya nyumba ya Bwana. 25 Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu, yule kahaba, na watu wa nyumba ya baba yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo; naye akakaa kati ya Israeli hata leo; kwa sababu aliwaficha wale wajumbe aliowatuma Yoshua ili kuupeleleza mji wa Yeriko.

 

Hadithi hii inamuonyesha kama Kanisa katika siku za mwisho. Kanisa litalindwa kwa sababu ya dhabihu iliyotolewa ya Mwanakondoo – Kristo. Kamba nyekundu inawakilisha damu yake kama ilivyotumika huko Misri kwenye milango na miimo ya milango. Hapa sio mahali salama, akama Rahabu alivyokuwa mahala pabaya sana alivyokaa – ukutani. Pia inaashiria ukweli kwamba emelindwa na kuwaokoa wale waliokuwa karibu naye wakati wa kuangamizwa na kupinduliwa kwa mataifa, kwa ajili ya uhusiano wake na Jeshi la Bwana kwa imani aliyokuwa nayo. Habari hii yote imeelezewa kwa kina kwenye jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 145) [The Fall of Jericho (No. 142)].

 

Mchakato huu wote ilifanyika kipindi chote cha Pasaka. Tangu siku ya kwanza ya Sikukuu hii walikula mazao ya nchi mpya ambayo ui kuhifadhi nafaka za mavuno ya zamani. Mana ilikoma na hawakuendelea tena kuitegemea hii mana huko jangwani na waliweza kuingilia kati mambo yao wenyewe kwenye Torati ya Mungu na imani.

 

Kama ilivyoelezwa hapo juu, baragumu zililazimu kupigwa kwenye Siku za Sikuu, Miandamo ya Mwezi, juu ya sadaka na kwenye sadaka za kuteketezwa ikionysha hii kuwa ni sehemu ya huu utaratibu wa maonyo ya Mungu. Zilitumika katika kuita na kuelekeza namna ya kuenenda katika kambi ya watu wa Mungu (Hesabu 10:2). Uhusiano wa wazi na wateule una kuonekana.

 

Kwa hiyo, baragumu zilivyotumika kwenye hadithi hii ya biblia, zinaashiria Mpango wa Mungu kutoka kwenye mtazamo mwelekezo wa maonyo ya Mungu yaliyotolewa kipindi cha zaidi ya miaka elfu sita. Mlolongo huu wa mambo unakuwepo kwenye kipindi cha ujio wa Kristo pamoja na mkusanyiko wa wateule wake atakapokuja. Hii itafuatiwa na kuangamizwa kwa mfumo wa dunia hii ulioonyeshwa kama hasira ya Mungu kwenye vitasa saba au majipu saba makuu na vita ya Siku Kubwa ya Mungu.

 

Ufunuo 11:15-19 Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele. 16 Na wale wazee ishirini na wanne waketio mbele za Mungu katika viti vya enzi vyao wakaanguka kifulifuli, wakamsujudia Mungu 17 wakisema, Tunakushukuru wewe, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa sababu umeutwaa uweza wako ulio mkuu, na kumiliki. 18 Na mataifa walikasirika, hasira yako nayo ikaja, na wakati ukaja wa kuhukumiwa waliokufa, na wa kuwapa thawabu yao watumwa wako manabii na watakatifu, na hao walichao jina lako, wadogo kwa wakubwa, na wa kuwaharibu hao waiharibuo nchi. 19 Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake. Kukawa na umeme, na sauti, na radi, na tetemeko la nchi, na mvua ya mawe nyingi sana.

 

Kwa hiyo, Siku ya Kwanza Takatifu ya mwezi wa saba inaitwa Siku ya Baragumu na inawakilisha Kurudi kwa Masihi akiwa kama Mfalme Mshindi kuja kuyatiisha mataifa.

 

Kuna uhusiano na Sikukuu za miezi ya Kwanza na Saba kama tutakavyoendlea kuelezea hapo chini. Siku Takatifu inayofuatia kunayoielezea kwenye mlolongo huu ni Siku ya Upatanisho.

 

Siku ya Upatanisho

Mambo ya Walawi 16:1-31 Bwana akasema na Musa, baada ya kufa kwa hao wana wawili wa Haruni, walipokaribia mbele za Bwana, wakafa; 2 Bwana akamwambia Musa, Sema na Haruni ndugu yako, kwamba asiingie wakati wo wote katika mahali patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, kilicho juu ya sanduku, asije akafa; maana, mimi nitaonekana katika lile wingu juu ya kiti cha rehema. 3 Haruni ataingia katika patakatifu na vitu hivi; ng'ombe mume mchanga kwa sadaka ya dhambi, na kondoo mume kwa sadaka ya kuteketezwa. 4 Ataivaa ile kanzu takatifu ya kitani, atakuwa na zile suruali za kitani mwilini mwake, atafungwa ule mshipi wa kitani, naye atavaa ile kofia ya kitani; hayo ndiyo mavazi matakatifu, naye ataoga mwili wake majini, na kuyavaa. 5 Kisha atatwaa mikononi mwa mkutano wa Waisraeli mbuzi waume wawili, kwa sadaka ya dhambi; na kondoo mume kwa sadaka ya kuteketezwa.6 Na Haruni atamtoa yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake. 7 Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweka mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania. 8 Na Haruni atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya Bwana; na kura ya pili kwa ajili ya Azazeli. 9 Na Haruni atamleta yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Bwana, na kumtoa awe sadaka ya dhambi. 10 Bali yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atawekwa hai mbele za Bwana ili kumfanyia upatanisho, ili kumpeleka jangwani kwa ajili ya Azazeli. 11 Na Haruni atamsongeza ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake; naye atamchinja yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake. 12 Kisha atatwaa chetezo kilichojaa makaa ya moto yatokayo katika madhabahu iliyo mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba mzuri uliopondwa sana, mikononi mwake, naye atauleta ndani ya pazia. 13 Kisha atatia ule uvumba juu ya moto mbele za Bwana, ili moshi wa ule uvumba ukisitiri kiti cha rehema kilicho juu ya ushuhuda, asije akafa. 14 Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng'ombe, na kuinyunyiza kwa kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba. 15 Kisha atamchinja yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya watu, na kuileta damu yake ndani ya pazia, na kwa damu hiyo atafanya vile vile kama alivyofanya kwa damu ya ng'ombe, na kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema, na mbele ya kiti cha rehema, 16 naye atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, kwa sababu ya mambo machafu ya wana wa Israeli, na kwa sababu ya makosa yao, naam, kwa ajili ya dhambi zao zote; naye atafanya vile vile kwa ajili ya hema ya kukutania, ikaayo pamoja nao katikati ya machafu yao. 17 Wala hapatakuwa na mtu katika hema ya kukutania, wakati aingiapo ili kufanya upatanisho katika patakatifu, hata atakapotoka nje, baada ya kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake, na kwa ajili ya mkutano wote wa Israeli. 18 Kisha atatoka na kuiendea madhabahu iliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake; atatwaa baadhi ya damu ya yule ng'ombe, na ya damu ya yule mbuzi, na kuitia juu ya pembe za madhabahu pande zote. 19 Tena atanyunyiza baadhi ya damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, na kuitakasa, ili machafu yote ya wana wa Israeli yaitoke. 20 Naye akiisha kufanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, na hema ya kukutania, na madhabahu, atamleta yule mbuzi aliye hai. 21 Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari. 22 Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani. 23 Na Haruni ataingia katika hema ya kukutania, naye atavua mavazi yake ya kitani, aliyoyavaa alipoingia katika patakatifu, atayaacha humo; 24 naye ataosha mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na kuvaa nguo zake, na kutoka, na kusongeza sadaka ya kuteketezwa yake mwenyewe, na sadaka ya kuteketezwa ya watu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu. 25 Na mafuta ya sadaka ya dhambi atayateketeza juu ya madhabahu. 26 Na mtu yule amwachaye mbuzi wa Azazeli aende zake, ataosha nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia katika marago. 27 Na yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, na yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, ambao damu yao ililetwa ndani ifanye ukumbusho katika patakatifu, watachukuliwa nje ya marago; nao watachoma moto ngozi zao, na nyama yao, na mavi yao. 28 Na yeye awachomaye moto atafua nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia maragoni. 29 Amri hii itakuwa amri ya milele kwenu; katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi, mtajitaabisha roho zenu, msifanye kazi ya namna yo yote, mzalia na mgeni akaaye kati yenu. 30 Kwa maana siku hiyo upatanisho utafanywa kwa ajili yenu, ili kuwatakasa; nanyi mtatakaswa na dhambi zenu zote mbele za Bwana. 31 Ni Sabato ya raha ya makini kwenu nanyi mtajitaabisha roho zenu; ni amri ya milele. 

 

Taratibu zote na maadhimosho ya Siku ya Upatanisho vimeelezewa kwa kina kwenye majarida ya Upatanisho (Na. 138) na Azazeli na Upatanisho (Na. 214) [Atonement (No. 138) and Azazel and Atonement (No. 214)].

 

Katika Siku ya Upatanisho kulikuwa na mbuzi wawili wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu. Kuhani Mkuu ndiye eke yake aliruhusiwa kuingia Patakatifu pa Patakatifu na aliruhusiwa kuingia hapo mara moja tu kwa mwaka katika hii Siku ya Upatanisho. Alioaswa aingie huko na sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe – ng’ombe dume – na alichukua damu ya mafahali na damu ya mmoja ya mbuzi katika Patakatifu pa Patakatifu. Tunajua kwamba hii ilikuwa inamlenga Kristo.

Weebrania 9:11-14 Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya ulimwengu huu, 12 wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele. 13 Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili; 14 basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?

 

Kuhani Mkuu, akiwa anafanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, watu na Patakatifu pa Patakatifu, nk, kisha alikiri na kuungama dhambi za watu juu ya kichwa cha mbuzi wa Azazeli. Kisha mbuzi aliondolewa mahali pale palipofurika watu na mwanaume mahiri su anayestahili.

 

Tunajionea mchakato wa namna hii hii wa upatanisho tunaouona katika mwezi wa Kwanza kwenye Utakaso wa Hekalu na kisha upatanisho na makuhani na watu kama ni wateule. Hapa mchakato ni upatanisho wa kuhani na hatimaye watu, kukafuatiwa na kuondolewa kwa Shetani. Kuhani alipatanishwa na Kristo, kwa mfano wa Yule dume wa ng’ombe, kuonyesha mabadiliko ya ukuhani. Kuondolewa kwa mbuzi wa Azazeli kunaasiria kitendo cha kufungwa kwa Shetani mwanzoni mwa kipindi cha Milenia. Watu wanapaswa kufunga saumu na “kuziteza nafsi zao” – inaonyesha utakaso na upatanisho. Kondoo waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa kuhani na watu wanaashiria majaribu na mateso ambayo tunapaswa kuyapitia. Tunajua kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya watu wote.

 

1Yohana 2:2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

 

Upatanisho huu unaendelea ili kuijumuisha sayari yote. Ni lazima ishike mkondo wake mapema kabla ya utawala wa Kristo. Kwa hiyo, Shetani lazima afungwe ili kuzuia ushawishi wake, kama ilivyoonyeshwa kwenye Ufunuo 20:1-3. Kristo alichaguliwa na kutengwa kando siku ya 10 ya mwezi wa Kwanza. Anautenga mbali ulimwengu kwa upatanisho na wongofu wa siku ya 10 ya mwezi wa Saba.

 

Idi ya Vibanda: majira ya mavuno ta tatu

Sikukuu ya Vibanda inafanyika kwa kipindi cha siku saba tu, ya kwanza ikiwa ni Sabato. Baada ya siku saba kukamilika au kwisha, siku inayofuatia ni Sabato. Siku hizi saba zinaashiria hitimisho, bali hizi sio Sabato ya siku ya saba ya juma. Ufanyaji wa kazi za kawaida wa siku ya saba ni ishara kufunguliwa kwa Shetani na harakati endelevu za Mungu kwenye mchakato. Siku Takatifu kwa hakika ni ile siku ya nane au Siku Iliyo Kuu nay a Mwisho ya Sikukuu au Siku ya Mkutano wa Makini. Kipindi cha siku saba inawakilisha kipindi cha miaka elfu saba. Sabato ya siku ya kwanza inaonyesha kufufuliwa kwa wateule wakati wa kurudi kwake Kristo. Sabato katika siku ya nane inaonyesha ufufuo wa mwisho utakaotokea baada ya kipindi hiki cha miaka elfu kikiisha na ujio wa Mji wa Mungu (tazama majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Mji wa Mungu (Na. 180) [The Resurrection of the Dead (No. 143) and The City of God (No. 180)].

 

Ufunuo 20:4-5 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. Huo ndio ufufuo wa kwanza

 

Kutoka aya ya 5 tunaona kwamba siku ya nane ni Ufufuo wa Pili wa wafu; ufunuo 20:4-5 inaonyesha Ufufuo wa Kwanza utakaotokea moja kwa moja baada ya miaka elfu. Siku ya Bwana ni kipindi chote kizima cha miaka elfu na kinaendela mbele kuhitimisha Siku ya Mwisho Iliyo Kuu ambayo ni kivuli au taswira ya Siku ya Mwisho Iliyo Kuu ya Sikukuu ya Vibanda ambayo kwayo watu wote watafufuliwa.

Yohana 6:39-40 Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho. 40 Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

 

Yohana 7:37-38 Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. 38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

 

Yohana 11:24-26 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho. 25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?

 

Yohana 12:48 Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.

 

Yohana 12:48 inaonyesha wale ambao hawajaitwa sasa (Yeye alikataae mimi na hayapokei maneno yangu) watakuwa na fursa nyingine katika Siku ya Mwisho – siku yao ya hukumu.

 

Kwahiyo, siku ya nane ni sehemu ya Sikukuu ya Vibanda na ni siku ya ufufuo wa watu wote. Siku ya nane pia ni Sabato kuu ya saba ya mwaka, kwa hiyo ni hitimisho na pumziko la Mungu kutoka kwenye utendaji wa kazi yake ya wokovu.

 

Majira haya ni Sabato ya juma la uumbaji, mavuno ya tatu ya Mungu.

 

Ufufuo wa Kwanza menenwa na Maandiko Matakatifu kuwa ndio ulio “bora”. Ni bora kwa sababu wale walio ndani ya ufufo huu watafufuliwa kwa uzima wa milele. Watakuwa wamekwisha hukumiwa tayari kabla ya ufufuo na kwa hiyo mauti ya pili hawana sababu ya kuiogopa. Wamefufuliwa milele na sio kwa hukumu au kwa maamuzi, kama wale walio kwenye Ufufuo wa Pili.

Yohana 5:29  Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.

 

Hawahitaji kufanya maamuzi wala kuhukumu kwa kuwa haya yamekwisha pita kwao. Ufufuo wa pili ni ufufuo wa hukumu na kufanya maamuzi au kukata shauri. Watu hawa hawajui wakati wa kufufuka kwao, ila wapende wasipende, wata watakumbwa na mauti ya pili. Wataishi kwa kitambo na kisha kuhukumiwa sawasawa na waliyoyafanya kipindi kile – maamuzi waliyoyafanya na maamuzi yaliyofanywa juu yao.

 

Hosea 5:14-15  Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama mwana-simba kwa nyumba ya Yuda; mimi, naam, mimi nitararua, kisha nitakwenda zangu; nitachukulia mbali, wala hapatakuwa na mtu wa kupokonya. 15 Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.

 

Hosea 6:1-2 Njoni, tumrudie Bwana; maana yeye amerarua, na yeye atatuponya; yeye amepiga, na yeye atatufunga jeraha zetu. 2 Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.

 

Aya hizi zinamahusiano ya Luka 13:32-33. Kwa hiyo zina maana kwenye huduma ya miaka mitatu ya Kristo. Pia ina uhusiano na mavuno ya Israeli, ambayo tumeyaona kwa suala la miaka mitatu ya mateso, sawa na kama Yuda walivyopitia mateso na mauaji makuu ya kimbari yanayojulikana kama Holocaust. Hata hivyo, hii ina maana ana zaidi ndani yake yanayohusiana na kipindi cha miaka elfu tatu ya mwisho (soma Hosea 6:2). Kipindi hiki kinafanya mabadiliko ya mfumo ukuhani mkuu kutoka ule wa Walawi kwenda kwa wa Melkizedeki (pia soma Hosea 5:14).

 

Kwa hiyo tunapaswa kuisoma Hosea 6:2, pale inaposema “baada ya siku mbili”, akimaanisha baada ya Alhamisi na Ijumaa, Jumamosi au Sabato. Hapa inahusiana na kufanyiwa “kuamshwa” na “kufufuliwa” katika siku hii. Kwa hiyo tunaweza kupunguza mlolongo nyakati za utoaji dhabihu na mateso kuwa ni kama siku tatu tangu kufa kwa Masihi na juma la Pasaka kama lilivyohusiana na mchakato wa miaka mitatu na wa miaka elfu tatu. Kipindi hiki kimehusishwa na kujumuishwa kwa miaka elfu mbili cha jangwani na miaka elfu moja ya utawala wa millennia na Yesu Kristo. Hii inaendana na Pentekoste ya arobaini (Yubile) kama kipindi chetu kirefu kabla ya mavuno makuu ya Mungu chini ya Masihi (Yeremia 5:24).

 

Kama ilivyoandikwa kwenye Mambo ya Walawi 23:42-43, Sikukuu ya Vibanda pia ilikuwa inafanya taswira kipindi cha Waisraeli walichotoka utumwani Misri na wakakaa kwenye Vibanda. Tutaweza kusema kwa ufupi tu kwamba sikukuu hii inahusiana na utokaji mpya kutoka utumwani wa tgaifa zima lote Isaya 66:20.

 

Isaya 66:20 Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi. 

 

Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ufupi tu kwamba maana yah ii ilikuwa inawahusu Israeli wa kimwili katika Milenia, kipindi hiki watakuwa kwenye maeelekezo au sheria za haki na watakuwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwao na ndipo watamtii Mungu na Torati yake ambazo zitakuwa ndiyo sheria na kanuzi za kuliongoza taifa na ni kipimo cha hukumu katika ufufuo wa mwisho wa wanadamu waliobakia.

 

Kwa hiyo kuna mahusiano mkubwa kati ya Sikukuu ya mwezi wa Kwanza na Sikukuu za mwezi wa Saba. Zinamaana kwa kila moja kwa nyingine kwa muundo unaotegemeana.

 

Tangu mwezi wa Kwanza hadi wa Saba

Mchakato huu wa marejesho ya kwanza umekusudiwa kufanywa na Masihi. Mlolongo wa mambo wa zama hizi umeelekezwa na mchakato uliopo kwenye mwezi wa Kwanza.

 

Katika siku ya kwanza ya mwezi, Utakaso wa Hekalu la Mungu unafanyika – Hekalu ambalo ni sisi (1Wakorintho 3:16; 6:19).

 

Aiku ya saba ya mwezi ni ya utakaso kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa kupotoshwa au bila kukusudia. Kufanya hivyo ni mumihu kwa ajili ya uumbaji wa viumbe vionekanavyo kwa sasa na kwenye Milenia na ni moja ya tofauti iliyopo kati ya miezi ya Nisan na Tishri, ambazo vinginevyo zinafanya taswira mpango huohuo na matendo yake.

 

Siku ya kumi ya mwezi wa Kwanza tunaona uchaguzi na kumtenga kando mwanakondoo ambaye anatangulia mchakato wa ukombozi na harakati kwa ajili ya malimbuko yanatolewa na yanakubalika na Mungu.

 

Siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza ni Sikukuu ya Pasaka. Marejesho yote kwenye zama hii yanaanzia tangu na yanahusiana na mwezi wa Kwanza yakiendelea hadi katika utoaji na ushiriki wa mlo wa mwili na damu ya Kristo ikiwa ni sakramenti ya pili ya wateule. Sakramenti ya kwanza ya wateule ni ubatizo, ambao ni awamu ya kwanza ya utakaso wa Hekalu. Kimsingi, hii inachukua nafasi yhake baada ya majira ya Sikukuu na baadae kidogo na kati ya siku ya 1 na ya 7 ya mwezi Nisani na kabla ya siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza.

 

Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu inakuwa ya siku moja na inafuatiwa na siku saba nyingine. Siku ya Kwanza Takatifu kenye sikukuu zote mbili inakuwa ni siku ya 15 ambayo kwa kawaida iakuwa ya mwezi kamili. Mchakato huu unaashiria dhabihu na maandalizi ya wateule kwa kuondoa dhambi na kisha kujijenga tayari kwa Pentekoste na Mavuno ya wateule Katika Yubile ya arobaini jangwani.

 

Kuna Siku Takatifu mwanzoni na mwishoni mwa Idi ya Mikate isiyo na Chachu, ambazo ni siku ya kwanza au Siku ya Pasaka siku ya 14 Nisani ikiwa ni siku ya maandalizo. Wateule wasipokuwa safi hawaruhusiwi kuula mkate usio na chachu wa Pasaka, ambao tumeuona kwenye Marejesho mapya (soma jarida la Marejesho ya Yosia (Na. 245) [Josiah's Restoration (No. 245)] wakati makuhani wa Mahali pa Juu hawakuruhusiwa kwenda Hekaluni kuila Pasaka. Kwa hiyo, ibada za sanamu ziliwatenga makuhani na kuwafanya wasistahili kuila Pasaka Hekaluni.

 

Tofauti iliyoko kati ya miezi hi yaw a Kwanza na wa Saba ni kwamba kusanyiko la Baragumu, na tena Miandamo ya Mwezi au siku ya Kwanza ya mwezi, inatangaza ujio wa Masihi kwenye harakati ya mambo ya dunia. Ataingia na kuzifupisha siku hizi kwa ajili ya wateule na uwepo wao na kuendelea wakiishika imani kama watu wa Mungu. Wanajulikana kwa matendo na kazi zao, zinaoendana na kuashiriwa na Sabato, iandamo ya Mwezi, Sikukuu na harakati zao tangu mwezi wa Kwanza na kuendelea na pamoja na kumpokea kwao Roho siku ya Pentekoste na Torati ya Mungu kwa ujumla.

 

Hakuna kufunga saumu katika siku ya saba ya mwezi wa Saba. Hakuna kile mtu anachokifanya leo kinacho fanana. Mwanakondoo amekwisha chinjwa tayari na kutolewa sadaka na kwa hiyo ufungaji saumu unafanyika siku ya kumi ya mwezi wa Saba wakati kwamba katika mwezi wa Kwanza umekuwa ukitengwa tu kwa ajili ya dhabihu inayotolewa siku ya 14.  Katika mwezi wa Saba, Yule Mwanakondoo aliyewekwa kando kule Mbinguni anarudi akiwa kama Mfalme Mshindi akitanguliwa na Baragumu au Tarumbeta, siku ya Kwanza ya mwezi wa Saba. Inapofika Siku ya Kumi ya Upatanisho, dunia inapatanishwa na kuandaliwa kwa utawala wa milenia.

 

Mataifa yanahukumiwa kwa mpangilio endelevu. Ni kama Yosia alipofanya marejesho ya Hekalu na Torati kutoka kwenye Pasaka na akaendelea zaidi kwa kipindi kisicho cha kawaida cha miaka kumi na mitatu baada ya mwaka 623/2 KK hadi alipokwenda Megido mwaka 609 KK kuyakabili mataifa na kufa, ndivyo vivyo hivyo ufalme utapita kutoka mikononi mwa wafalme hadi mikononi mwa Masihi, anayestahili.

 

Sikukuu ya \Mkusanyiko inatakiwa iende sambamba na utoaji wa sadaka jioni ya siku ya kwanza ya Sikukuu. Siku ya kwanza ya idi ya Vibanda ni Takatifu, kwa hiyo hakuruhusiwi kufanya kazi yoyote na wanadamu zaidi ya kutoa sadaka ya kusanyiko, ambayo haitakiwi ibakie hadi asubuhi.

 

Siku saba za Vibanda zinafananishwa na millennia nazo zinakuwa saba sawa na siku za Mikate Isiyo na Chachu. Kwenye mfano wa kwanza, Masihi alikufa ili kuiwezesha Sikukuu ya Pasaka. Matendo ya wanadamu yanapaswa kuondoka duniani.

 

Katika mwezi wa Saba, Sikukuu inaashiria utawala wa Masihi kwenye hii sayari ambako hakuna ulazima wa kutoka na kuiacha dunia, kwa kuwa ulimwengu wote utakuwa kwenye jutawala wa haki na maongozi ya Torati ya Mungu.

 

Kwa hiyo, siku ya saba ya Idi ya Vibanda sio siku takatifu, kwa kuwa inaashiria dunia kurudi kwenye Ibilisi Msitaki wetu na kipindi cha vita.

 

Kwa upande mwingine, Siku ya Mwisho Ilikyokuu ni siku ya nane, ambayo ni tofauti kabisa na siku za Mkate Usio na Chachu, iko mwishoni na siyo mwanzoni na ni Siku Takatifu. Paska kwa namna nyingine sio Siku Takatifu kwa sababu kwa kuwa inaziwakilisha kazi za Masihi kwa wokovu wa mwanadamu.

 

Siku ya MWisho Iliyo kuun ni Takatifu kwa kuwa inawakilisha hukumu ya haki kwa ulimwengu na kuondolewa dhambi mara ya mwisho katika historia. Inawakilisha ujio wa Mungu Ulimnwenguni na kushuka kwa |Mji wa Mungu vikiungana kwa marejesho ya mwisho.

 

Haya marejesho ya mwisho ni hitimisho ya mwisho ya Mpango wa Mungu.

 Marejesho mapya ya dunia katika Mpango wa Mungu kama yalivyoashiriwa na maadhimisho ya Sikukuu na Siku Takatifu na utaratibu wake, yameelezewa kwa kina kwenye majarida ya Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241), Utakaso Kwa Ajili ya Dhambi za Kupotoshwa (Na. 291) na  Sabato Kuu Saba (Na. 107 [Sanctification of the Temple of God (No. 241); Sanctification of the Simple and Erroneous (No. 291); Josiah's Restoration (No. 245) and The Seven Great Passovers of the Bible (No. 107)]. Sikukuu hizi na Siku Takatifu hizi zote zina maana yake kwa harakati zake kwenye mchakato wa Mpango wa Mungu.

  


 

Ukurasa wa Nyongeza kwenye jarida hili Namba 227

 

Alhamisi, siku ya 1 Nisani:  Mwandamo wa Mwezi na Siku ya Kwanza ya Mwaka Mtakatifu. Utakaso wa Hekalu ulifuatia baada ya siku hii (Ezekieli 45:18; sawa na jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [Sanctification of the Temple of God (No. 241)]. Mwandamo wa Mwezi uliadhimishwa wakati wa kipindi chote cha huduma ya Kikuhani Hekaluni, pamoja na utoaji wa sadaka za siku za Sabato na Siku Takatifu (kwa mujibu wa Josephus, Wars of the Jews, Bk. V, ch. V, 7). Katika siku za Miandamo ya Mwezi, hususan siku hii, na Sabato na Sikukuu, Kuhani Mkuu alipanda kwenda Hekaluni pamoja na makuhani wengine.

 

Jumatano, siku ya 7 Nisani: (siku 8 kuifikia Pasaka na mwisho wa juma la kwanza na la Utakaso la mwaka0). Utakaso kwa ajili ya Dhami zilizofanywa kwa ujinga na kupotoshwa (Ezekieli 45:20; sawa na jarida la Utakaso Kwa Dhambi za Kupotoshwa (Na. 291) pSanctification of the Simple and Erroneous (No. 291)]. Kristo anaandaliwa. Anautakaso kwa ajili ya wote kwenye Pasaka hii.

 

Alhamisi, siku ya 8 Nisani:  (siku 7 kuifikia Pasaka) Kristo anaingia mjini Yerusalemu alitokea Yeriko. Anashinda usiku nyumbani kwa Zakayo (Luka 19:1-10).

 

Ijumaa, siku ya 9 Nisani: (siku 6 kuifikia Pasaka) (vitu vyote kueoka hapa vimeelezewa kwa kina kwenye jarida la Wakati wa Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159( [Timing of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)].

 

Kristo anaingia kwa mara ya kwanza akitokea Bethfage (sio Bethania; sawa na Mathayo 21:8-9). Hakutarajiwa. Analisafisha Hekalu sawasawa na maagizo ya Torati (sawa na Mathayo 21:12-16). Anaondoka kwenya Bethania na anaadhimisha Sabato huko. Mariamu anampangusa miguu yake Bwana Yesu kwa manukato (Mathayo 21:1-9; Yohana 12:1).

 

Jumamosi, siku ya 10 Nisani:  (siku 5 kuelekea Pasaka)

Kristo anaishika Sabato huko Bethania. Anateuliwa na kutengwa kama Mwanakondoo (Yohana 12:2-11).

 

Jumapili, siku ya 11 Nisani: (siku 4 kufikia Pasaka)

Anaingia kwa shangwe mjini Yerusalemu akitokea Bethania. Yesu anaingia na kulikagua Hekalu kissa anarudi Bethania (Marko 11:1-11; Luka 19:29-44; Yohana 12:12-19).

 

Jumatatu, siku ya 12 Nisani:  (siku 3 kufikia Pasaka)

Kristo anarudi asubuhi anatokea tena Hekaluni na analisafisha.

Anarundi Hekaluni (Mathayo 21:18-22; Marko 11:12-19; Luka 19:45-48).

 

Jumanne, siku ya 13 Nisani:  (siku ya 2 kufikia Pasaka)

Kristo anakuwa tena mjini Yerusalemu. Anafundisha kwa njia ya maswali na mafumbo. Unabii juu ya Hekalu na mafuta ya Mzeituni yanatolewa. Ilipofika kuzama kwa jua Kristo anawaambia wanafunzi wake waende Yerusalemu wakatafute mahali na kuiandaa Pasaka (Mathayo 21:23-39; 24:1-51; 25:1-46; 26:17-20; Marko 11:20-33; 12:1-44; 13:1-37; Luka 20:1-21:38).

 

Jumatano, siku 14 Nisani:  (siku 1 kuelekea Pasaka; siku ya/1 ya Mikate Isiyo na Chachu)

Mlo wa usiku wa Jumatano halafu Ushirika wa Meza ya Bwana au Pasaka, Kuoshana miguu, kusalitiwa, nk.

Majira ya mchana – kusalitiwa, nk, halafu Kusulibiwa.

Kristo anapelekwa chini mtini na anazikwa kaburini kabla ya jua kuzama (kuanza kwa Sabato ya Pasaka) (Mathayo 26:20-27:66; Marko 14:17-15:47; Luka 22:14-23:55; Yohana 13:1-19:42).

 

Alahamisi, siku ya 15 Nisani

PASAKA/SIKU YA 1 ya MIKATE ISIYO NA CHACHU

Majira ya usiku – Siku ya 1 usiku kaburini. Majira ya mchana – siku ya 1 kaburini.

 

Ijumaa, siku ya 16 Nisani

Majira ya usiku – usiku wa 2 kaburini. Majira ya mchana – siku ya 2 ksburini.

 

Jumamosi, siku ya 17 Nisani

Majira ya usiku – usiku wa 3 kaburini. Majira ya mchana – siku ya 3 kaburini.

Majira ya alasiri, Kristo Mungu anamfufua Kristo kutoka kwa wafu.

 

Jumapili, siku ya 18 Nisani

SADAKA YA MGANDA WA KUTIKISWA INATOLEWA

Kristo anapaa kwenda mbinguni kwa Baba yake ambaye ni Mungu wake ili akubalike kama sadaka kwa ajili ya dhambi zetu (Mathayo 28:1-7; Marko 16:1-7; Luka 24:1-9; Yohana 20:1-9; 20:16-17).

 

q