Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[119]

 

 

 

Ukoo wa Uzao wa Masihi

(Toleo La 2.0 19950604-20050509)

 

Maana ya mstari wa ukoo wa Masihi imefafanuliwa kutoka Adamu. Maandiko yaliyo kwenye Mathayo 1 na Luka 3 yanaelekezewa na kufafanuliwa na mkanganyiko wake uliopo kati yao na kwenye kitabu cha Nyakati kumefafanuliwa pia. Maana halisi na sahihi yanaonyesha kwamba kwa kweli Masihi alitumwa ili kuwaokoa wenye dhambi.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 1998, 2005  Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Ukoo wa Uzao wa Masihi

 


Ukoo wa Masihi ni kitu muhimu sana ili kuelewa Masihi alikuwa ni yupi. La muhimu zaidi ni kwamba uzao wake huo unaleta maana ya muhimu sana ya utimilifu wa unabii na pia ya sheria ya kibiblia. Kufutwa yake kwenye tafsiri ijulikanayo kama the Reader’s Digest Bible ni makosa makubwa sana nay a bahati mbaya sana.

 

Kuna idadi kadhaa ya kanuni za mstari wa kiuzao zinazotakiwa kueleweka pia kutokana mpangilio wa nje. Ya kwanza ni ile ambayo kwamba ni wanawake tu ndio wanaopitiwa kwao. Hii inatokana na sheria na tendo la kwamba mwanamke anakuwa amechukuliwa na kuingizwa kwenye kabila la mume wake anapoolewa. Kulikwa na idadi kadhaa ya sheria, zilizokataza matendo ya kuoana watu wa jamii moja. Makatazo ya kitendo hiki cha kuoleana ndani ya ukoo mmoja yalikuwepo kwa sababu za maana sana. Kutokana na Hesabu 36 tunaona kwamba ardhi ilitolewa kwa ajili ya urithi kwa kuipigia kura wakipewa wana wa Israeli. Urithi uligawiwa kwa kigezo cha wazawa wa ukoo husika. Hakuna mwanamke aliyepewa urithi wa makabila ya Israeli angaliyeweza kuolewa nje ya kabila lake (Hesabu 36:8). Bali alikuwa ni budi aolewe kwenye familia ya ya kabila la baba yake. Urithi wake usingeweza kuondolewa kutoka kabila moja hadi jingine. Kila kabila liliwajibika kuuzingatia urithi wao (Hesabu 36:9). Kwa kuutangaza mwaka wa Yubile ndipo urithi uliorithiwa ulitolewa na kupewa kabila ambalo mwanamke huyu ameolewa kwalo (Hesabu 36:4). Sheria za mwaka wa Yubile zilitendeka kwa mujibu sawa na zilivyoagizwa kwenye Mambo ya Walawi 25. Kwa hiyo basi mstari wa uzawa ulikuwa ni wa muhimu ili kuelewa na kurekebisha utaratibu wa kiuchumi chini ya torati. Utaratibu huu unadaiwa kuwa kuanikizwa wakati wa utawala wa Masihi (soma kitabu cha nabii Ezekiel kuona jinsi utakavyoendelea). Mungu anafuata mistari ya damu ya kiuzao na kuwalinda hata kipindi cha utawaniko na hata kile cha kwenda kwao utumwani (Amosi 9:9).

 

Kanuni hizi za urithi zinawahusu pia Walawi. Nyumba za miji ya Walawi zilikuwa ni mali yao katika mwaka wa Yubile. Kwa huyo Walawi walihusishwa kwenye sheria hizi za urithi kwa makundi yote mawili, yaani kwa makuhani na kwa miji na kwa mashamba ya viungani mwa miji (Walawi 25:32-34). Maelekezo haya ya Walawi yanauhusuano na unabii kuhusu Masihi, kama tutakavyokwenda kuona.

 

Mstari wa uzao wa Masihi kwenye Agano Jipya unajiri na mistari miwili, kwenye Mathayo 1:1-7 na Luka 3:23-38, na mistari miwili yote inatofautiana kabisa. Zaidi sana, ni kwamba mstari ulio kwenye Mathayo unatofautiana na jinsi ilivyo kwenye kitabu cha Mambo ya Nyakati. Kwa hiyo, kunahitajika maeelezo na ufafanuzi wa kina kwenye mikanganyiko hii, au vinginevyo basi Biblia ichukuliwe kuwa haina nguvu yoyote ya uvuvio. Ukristo wa sasa umeamua kupuuzia tatizo hili kiasi cha hata kwenda kwenye uhafidhina tunaouona kwenye kitabu cha Reader’s Digest Bible. Ili kujua kinachotokea ni kuyakubali matatizo mengine ambayo wengine wameamua kuyapuuzia.

 

Mathayo na Luka wote wawili wanaanza na Adamu. Mstari ni mchakato wa kushusha chini umuhimu wa unabii wa familia fulani kwa kipindi fulani. Uzao wa mwanamke alitokea kwa na Adamu (Mwanzo 3:15). Uzao huyu wa mwanamke hapa ni mmoja wa kike (zer’a). (Maandiko ya Mwanzo 17:7; 21:12; na Wagalatia 3:16 yanafanana. Uweza au nguvu za Shetani zinaondolwewa na utawala wake utaangamizwa kutokana na Waebrania 2:14; 1Yohana 3:8).

 

Mwanzo 17:7 inaonyesha kwamba Agano na kwamba yampasa Masihi aje kwa kupitia uzao wa Ibrahimu. Mwanzo 21:12 inauonyesha mstari wa Isaka ambao kwamba uzao wa Utaitwa. Hata hivyo, Ishimaeli alikuwa pia ni wa uzao wa Ibrahimu na kwa hiyo kulianzishwa taifa. Hata hivyo, ilikuwa ni kwa kupitia Isaka ndipo uzao huo uliitwa.

 

Mstari wa Masihi unaelekezwa zaidi. Yohana 7:42 inaelezea idadi ya unabii kwenye andiko moja.

Yohana 7:42 Andiko halikusema ya kwamba Kristo atoka katika uzao wa Daudi, na kutoka Bethlehemu, mji ule alioukaa Daudi?

 

Maandiko Matakatifu yanayojiri na maandiko haya yanakutkana kwenye Zaburi 110:1-7 ambapo kuna Bwana wa Daudi na Kuhani Melikizedeki. Andiko hilo linamhusu Masihi kuhani.

 

Zaburi 132:6,11 inaonyesha kwamba Daudi na Efraimu kwamba Mungu ataketi kwenye kiti cha enzi.

Zaburi 132:11 Bwana amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalihalifu, Baadhi ya wazao wa mwili wako Nitawaweka katika kiti chako cha enzi.

 

Masihi atatokana na nyumba ya Yese ana atakuwa ni wokovu wa Mataifa kutokana na Isaya 11:1,10.

Isaya 11:1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.

 

Isaya 11:10 Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

 

Kwa hiyo, Masihi ilimpasa awe ni wa uzao wa Yese, baba wa Daudi. Masihi anatokana na mstari wa uzao wa Daudi kwa mujibu wa Yeremia 23:5-8.

Yeremia 23:5-8 Tazama siku zinakuja, asema Bwana, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi. 6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, Bwana ni haki yetu. 7 Kwa hiyo, angalia, siku zinakuja, asema Bwana, ambapo hawatasema tena, Aishivyo Bwana, aliyewatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri; 8 lakini, Aishivyo Bwana, aliyewapandisha na kuwaongoza wazao wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini, na kutoka nchi zote nilikowafukuza; nao watakaa katika nchi yao wenyewe.

Andiko hili linakanganya Ukristo wa kisasa kwa kuwa linaonyesha kwa dhahiri sana kwamba Masihi atatawala hapa duniani na kwamba kutakuwa na tukio la pili la Kutoka litakalowaimarisha Israeli na kuanzishwa kwa taifa lao.

 

Mika 5:2 inaonyesha kwamba Masihi atazaliwa Bethlehemu.

Mika 5:2 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

 

Kwa hiyo, uzao wa mwanamke ni wa Adamu kupitia Ibrahimu, kupitia kwa Isaka, kupitia kwa Yuda, kupitia kwa Daudi na ni kutoka Bethlehemu. Haya ni maelekezo ya kimapokeo ya mstari huu. Mstari huu unaweza kuelezewa zaidi kuliko hivi.kuna mambo mawili kuhusu ujio wa Masihi yanayoonyesha kwamba Masihi atakuwa na aina mbili za marejeo kwa madhumuni mawili. Lengo la kwanza ni kwamba yeye ni kuhani Masihi kuanzisha ukuhani wa mfano wa Melkizedeki, ili kufanya huduma ya kikuhani tsiotokana na uzao, ili kwamba iweze kufunguliwa kwa Wamataifa kama zawadi au kipawa toka kwa Mungu.

 

Watakatifu wamesamehewa na kufutiwa makosa yao na Kristo na kufanyika kuwa wafalme na makuhani (Ufunuo 1:6; 5:9-10).

Ufunuo 5:9-10

Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, 10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.

 

Ukuhani wa Haruni kwa hiyo unapasa kufikia mwisho na pamoja nao hata kwenye Mahekalu yote mawili, yaani lile la Yerusalemu na lile la Misri lililoko huko Heliopolis. Hekalu la Leontopolis kwenye lakabu ya Heliopolis lilianzishwa na kujengwa na Onias IV kwa kupitia unabii ulio kwenye Isaya 19:19. Lilijengwa kwenye ardhi ya Gosheni ili kusaidia kutimilika kwa unabii wa Hosea uliotolewa kwa kuwalenga wote wawili, yaani Israeli na Mesihi, uliosema, Nikamwita mwanangu atoke Misri (Hosea 11:1; Mathayo 2:15). Hekalu lililokuwa huko Misri lilifanya kazi tangu mwaka 160 KK hadi mwaka 71 BK wakati lilipofungwa kwa amri iliyotolwa na Vespasian baada ya kuangamia kwa Yerusalemu. Kwa hiyo kufungwa kwake kulihitimisha unabii wa Yona, uliodumu tangu mwaka 30 BK - 70 BK, na kisha ukatimilika tangu siku ya 1 Abibu, mwaka 70 BK hadi siku ya 1 Abibu, mwaka 71 BK (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Kuangamizwa kwa Hekalu (Na. 13)). Mamlaka ya hekalu yaliondolewa baada ya miaka arobaini kwisha ambayo iliruhusiwa kwa ajili ya kuwapa Yuda muda wa kutunu. Miaka arobaini iliyofuatia kutoka miaka mitatu ya huduma ya Masihi kwa hesabu ya kuufananisha mwaka mmoja sawa na siku dhidi ya ile huduma ya Yoha huko Ninawi.

 

Amri mpya ilikuwa ni baada ya Melkisedeki (Zaburi 110:4). Kristo alikuwa Kuhani Mkuu wa utaratibu ule. Wateule ni makuhani, wasiotokana na mstari wa uzao (Waebrnia 7:1-21). Makuhani hawa wanakuwa pia ni wafalme waliopewa ufalme (Waebrania 12:28). Ni ushahidi unaojitegemea kwamba Kuhani Mkuu anaweza pia kuwa hivyo kama kuna makuhani wengine ambao anaoweza kuwatawala. Kwa kutafsiri au kumaanisha twaweza kusema kwamba hao hawawezi kuwa ni wa Haruni, ingawaje wana wa Haruni nao watakuwa ni sehemu ya ukuhani huu (Ufunuo 7:7). Dhana ya ukuhani ni pana zaidi kuliko taifa, kama dhana ya Israeli ilivyopanuka na kujumuisha mataifa yote.

 

Mstari wa uzao wa Masihi haukuujumuisha mstari wa Daudi tu bali pia na ule wa Haruni. Unabii unaonyesha kwamba mistari hii ilikuwa ni ya Daudi kwa kupitia Nathan na Lawi kupitia kwa Shimei. Unabii huu upo kwenye Zekaria 12:10-14 pia unaonyesha kwamba Masihi alipaswa kuuawa.

Zekaria 12:10-14 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido. 12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao. (kumbuka kwamba tafsiri ya KJV inasomeka kwamba mimi smbsye wamemchoma ikituama kwenye nahau za kimagharibi, nahau za kimashariki neno sahihi ni kuwa yeye).

 

Andiko hili linaonyesha mistari miwili ya uzao. Wa kwanza ni wa Daudi kupitia Nathani na wa pili ni wa Lawi kupitia kwa Shimei. Kitendo hiki kilisababisha maangamizi na maombolezo ya Yerusalemu kama taifa (aya za 11-14). Kwa hiyo unabii uliendana na maangamizo ya Yerusalemu hadi kifo cha Masihi. Kipindi cha muda uliotolewa wa miaka arobaini tangu mwaka 30 BK hadi mwaka 70 BK kwa hiyo kina maana yake fulani. Yerusalemu ilizingirwa na majeshi ya Kirumi tangu siku ya 1 Nisan, mwaka 70 BK. Hekalu la Yerusalemu  liliangamizwa mwaka wa 70 BK tangu siku ya Upatanisho, hata hivyo, hekalu la Misri liliamriwa kufungwa mwaka uliofuatia wa 71 BK kwa amri ya Vespasian kukifuatiwa na vita ya Wayahudi. Maangamizo yaliendelea nchi nzima baada ya kuangamizwa kwa hekalu.

 

Ni kina Mathayo na Luka tu ndio wanaohusisha au kuuelezea mstari huu wa uzao wake. Marko na Yohaya wanaanzia kwa kumuelezea Yesu akiwa ,kubwa, kwa hiyo mstari wao wa uzao hauwezi kufanana

 

Kwenye jarida lake (la “The Genealogy of Messiah (Mstari wa Uzao wa Masihi)”, The Vineyard (Shamba la Mizabibu), November 1993, kurasa za 10-13, lililochapishwa tena kutoka kwenye lijulikanalo kama Issues, A Messianic Jewish Perspective), Dr. Arnold Fruchtenbaum wa Ariel Ministries anasema hivi:

Kwenye Mathayo, Yusufu alifanya kazi nzuri na ya muhimu, lakini Mariamu (Maria) alifanya kazi hodari kabisa. Mathayo anaandika habari kuhusu malaika walimtokea Mariamu, Mathayo ameandika kuhusu mawazo aliyokuwanayo Yusufu lakini hakuna kilichpandikwa kuhusu alichokuwa anawaza Mariamu.  Kwa upande mwingine, Injili ya Luka inaelezea habari hiyohiyo kwa mtazamo wa Mariamu. Kwa mtazamo wa kila Injili, ingekuwa ni wazi na shahiri sana kwamba maelezo ya Mathayo kuhusu mstari huu wa uzao ni kwamba wa Yusufu, na maelezo ya Luka ni kwamba wa Mariamu.

 

Ndipo linapoibuka swali la kwamba: ni kwa nini tunahitaji kuwa na mistari miwili ya uzao, hususan kwa vile Y’shua (Yesu) hakuwa mwana hasa wa Yusufu? Jibu lijulikanalo sana na la kawaida ni kwamba: Injili ya Mathayo inatoa mstari wa kifalme, wakati ile ya Luka ikitoa mstari halisi na wa kweli. Kutokana na dhana hii ndipo dhana nyingine inaibuka. Kwa kuwa Yusufu anaonekana kuwa ni mrithi mstahili wa kiti cha enzi cha Daudi, na Yesu alikuwa ni mtoto wa kumlea tu na sio wa kumzaa mwenyewe Yusufu, basi Yesu angeweza kudai haki kwenye kiti cha enzi cha Daudi.

 

Kwa upande mwingine ni kwamba Injili ya Luka inatoa kipindi halisi, kuonyesha kwamba Y’shua mwenyewe alikuwa ni wa uzao wa Daudi. Kwa kupitia Mariamu, alikuwa mshiriki kwenye nyumba ya Daudi, lakini angeweza kudai haki ya kuketi kwenye kiti cha enzi cha Daudi kwa kupitia Yusufu, anayestahili kabisa. Kwa kweli kabisa, kinyume chake ndiyo ukweli (msisitizo umeongezewa).

 

Arnold Fruchtenbaum anaibua mambo ya muhimu sana kwenye kitabu chake, hata hivyo, hayashikilii na kuyachukulia kuwa ni mambo ya muhimu sana kwenye kuelewa kuhusu Zakaria kama tunavyoona hapo juu. Kutokana na Zakaria tunaona mstari wa uzao wa Daudi kwa kupitia Nathani ikitajwa. Hakuna kilichotajwa kuhusu Daudi kupitia kwa Sulemani na kwa sababu njema sana.

 

Kama ilivoelezwa na Fruchtenbaum, kulikuwa na masharti mawili ya uhusiano wa kidugu kwenye Maandiko Matakatifu ya Kiebrania. Hawa waliasiliwa baada ya kugawanyika kwa ufalme baada ya kufa kwa Sulemani.

 

Sharti la muhimu la kuchukua kiti cha enzi cha ufalme wa Yuda lilikuwa ni kuwa mtu anayetoka kwenye ukoo wa Daudi. Masihi alipaswa kuketishwa kwenye kiti cha enzi cha Daudi (Isaya 9:7). Mfalme alipaswa atokane tu na Nyumba ya Daudi. Yeremia 33:20-21 inaonyesha kwamba agano na Daudi na uzao wake, na pia na Walawi, halikuwezekena kuvunjika. Hila yoyote ya kutangua na kuondolea mbali nyumba ya Daudi kama tunavyoona kwenye Isaya 7:5-6 ilitabiriwa kuwa itashindwa.

Isaya 7:5-6 Kwa kuwa Shamu amekusudia mabaya juu yako, pamoja na Efraimu na mwana wa Remalia, wakisema, 6 Haya, na tupande ili kupigana na Yuda na kuwasumbua, tukabomoe mahali tupate kuingia, na kummilikisha mfalme ndani yake, huyo mwana wa Tabeeli.

 

Kushindwa kulikotabiriwa kulimaanisha kuulinda ufalme ili kwamba Maandiko yasitanguke. Masihi atarudi ili kuuchukua ufalme huo sawasawa na ilivyoandikwa kwenye Danieli 2:35,44-45.

 

Kushindwa kwa njama zozote zile kumeonekana kwenye Isaya 8:9-15 ambako kunasema kuwa ni Mungu tu ndiye astahiliye kuogopwa na ndiye wa kumcha.

Isaya 8:9-15 Fanyeni ghasia, enyi kabila za watu, Nanyi mtavunjwa vipande vipande; Tegeni masikio, ninyi nyote wa nchi zilizo mbali; Jikazeni viuno, nanyi mtavunjwa vipande vipande; Jikazeni viuno, nanyi mtavunjwa vipande vipande. 10 Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi. 11 Maana Bwana aliniambia hivi, kwa mkono hodari, akanifundisha nisiende katika njia ya watu hawa, akisema, 12 Msiseme, Ni fitina, katika habari za mambo yote ambayo watu hawa watasema, Ni fitina; msihofu kwa hofu yao, wala msiogope. 13 Bwana wa majeshi ndiye mtakayemtakasa; na awe yeye hofu yenu, na awe yeye utisho wenu. 14 Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu. 15 Na wengi watajikwaa juu yake, na kuanguka na kuvunjika, na kunaswa na kukamatwa.

 

Yeyote aliyejaribu kutawala kwenye kiti cha enzi cha Israeli bila kuruhusiwa na Mungu alikumbwa na maafa makubwa. Wote waliojitwalia kiti cha enzi cha ufalme wa Samaria pasipo kuruhusiwa na unabii waliuawa kwa ghafla (1Wafalme 11:26-39; 15:28-30; 16:1-4,11-15; 21:21-29; 2Wafalme 9:6-10; 10:29-31; 14:8-12).

 

Andiko linguine la maana na muhimu sana na lakini lililokataliwa na kutotilliwa maanani linalohusiana na watu wa nyumbani mwa Daudi kwa Masihi ni Zekaria 12:7-9 linalotanguliwa na lile lililonukuliwa hapo juu lakini kwa kweli linawekwa kwenye mkururo ulio nyuma ya harakati zilizotajwa kwenye Zekaria 12:10-14. Zekaria 12:10-14 inahusiana na kuuawa kwa Masihi wakati alipokuja mara yake ya kwanza. Andiko lililoko hapo juu lipo kwenye Zekaria 12:7-9 linahusiana na kurudi kwake na vita vya nyakati za mwisho.

Zekaria 12:7-9 Naye Bwana ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili utukufu wa nyumba ya Daudi, na utukufu wa wenyeji wa Yerusalemu, usipate kutukuzwa kuliko Yuda. 8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao. 9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu.

 

Jambo la muhimu kwenye andiko hili ni kwamba:

1.    Yuda ameongoka na kuokolewa kwenye kutangiliwa ili kwamba utukufu wa Nyuma ya Daudi na pia kwamba kwa Yerusalemu hautukuzwi kinyume na Yuda.

2.    Yerusalemu utalindwa na Bwana. Yeye aliyedhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi; na Nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana [Yehova] mbele yao.

3.    Katika siku hiyo mataifa yote ambayo yalikuwa kinyume na Yerusalemu yataangamia.

 

Vifungu hivi ni vya muhimu sana. Ili kuvielezea vifungu vya mwisho kwanza, ni wazi sana kwamba tunatatizwa na siku za mwisho na vita vya kinabii vya Bonde la Megido kwenye aya ya 11. Hivyo basi, tukio la mauti ya kwanza linatumiwa ili kuakinisha ushindi wa mwisho dhidi ya mataifa.

 

Mambo mawili ya kwanza yanaonyesha kwamba kuna tofauti iliyofanya tofauti kati ya Nyumba ya Daudi na kwamba ile ya Nyumba ya Yuda ambapo kiuzoefu majira mamoja ya machipuko hadi mengineyo. Hata hivyo hilo si kitu sana kwa watu wa Nyumbanimwake Daudi katika nyakati za mwisho kwa kuwa imeenea hadi kuwajumuisha Wamataifa chini ya watakatifu kama tulivyoona hapo juu ambapo Wamataifa wanazirithi baraka kwa kupitia Masihi.

 

Mkururo huu unaonyesha kiwango cha kimwili na cha kiroho. Kwanza kabisa, udhaifu wa Yerusalemu utatiwa nguvu na kuwa kama Daudi. La pili, wakazi wa nyumbani mwake kwenye kipindi hiki watakuwa kama Elohim au Mungu, kama Malaika wa Yehova (au Yahova) aliyekuwa mbele yao. Malaika wa Yehova alikuwa ni Malaika Mkuu wa Ushauri anayetajwa kwenye tafsiri ya LXX, kwenye Isaya 9:6, mungu wa pili wa Waisraeli ambaye ni Malaika wa Yehova (au Yahova) wa Zekaria 12:8. Malaika huyu alikuwa ni elohim na alikuwa ndiye uso wa Mungu, ni Penieli wa Mababa wa imani, ni El Betheli au Mungu wa Nyumba ya Mungu wa Ibrahimu. Malaika huyu alikuwa ni Mungu aliyemtia mafuta kama ni Mungu na Mungu wake kwa mafuta ya furaha juu ya ndugu zake kwa mujibu wa Zaburi 45:6-7 ambaye Waebrania 1:8-9 inatuonyesha kuwa inamtaja Masihi.

 

Hivyo watakatifu wanafanyika kuwa elohim, kama Kristo alivyo elohim, kama mtangulizi wa Malaika wa Yahovah wa Agano la Kale, na ni kama elohim kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu akiwa kama mwana wa Mungu mwenye mamlaka (Warumi 1:4; Waebrania 1:8-9).

 

Hii ni dhana yenye nguvu sana. Inaonysha pia ukubwa wa wito wa Mungu na mpango wa Mungu. Imekataliwa kwa kuwa haifanyi kwa mujibu wa mitizamo ya kihafidhina ya Mtaguso wa Kalkedoni uliofanyika takriban mwaka 451.

 

Kwa hiyo tupo kwene mahala muafaka kuhusianisha na Mathayo na Luka na Maandiko mengineyo kwenye mstakabala wake sahihi. Mstari wa uzao wa Masihi ulio kwenye Mathayo una idadi kadhaa ya mabo yanayotofautiana ambayo inaibua mikururo ya mafundisho ya biblia na kuonyesha kikamilifu kabisa sababu ya ni kwanini mstari ule yapasa uwe ule wa Yusufu. Y’shua au Yoshua asingeweza kuwa Masihi kwa kuhesabiwa tu hivyo na Mathayo peke yake. Hesabu iliyo kwenye Luka inahitaji kuonyesha ni kwa nini licha ya mstari wa Yusufu, angefanyika kuwa mfalme na jinsi Mungu alivyohusika kupatanisha kwa amri au shauri alilolianzisha kwenye mstari wa Daudi na ufalme kwa kupitia nabii Yeremia.

 

Masihi ametajwa kwa maelekezo ya mbingu. Jina lake limetolewa kwenye Mathayo 1:21 na Luka 1:31. Jina limechukuliwa au linatokana na jina la Hoshea (kama ilivyo kwenye Hesabu 13:16) ambalo kiambishi chake cha Yah kinatamkwa au kuandikwa Jah. Hii inamaanisha kabisa kwamba Mungu ni Wokovu wetu. Kwa hiyo Yahoshua linatumika kama Yeshua au Yoshua linapotumika, Yesu au Jesus ni uitaji wa Kiyunani wa jina Yoshua na linatokana na chimbuko lisilo la Kiebrania. Muundo kwenye Kiyunani unawezekana kabisa kushawishika au kufananishwa na Esus wa imani ya utatu aliyekuwa anaabudiwa kwenye Dini za Wahyperboreani.

 

Mathayo anauanza mstari huu kwa kuyakinisha mambo makubwa matatu ya muhimu. Yeshua au Yoshua anayeitwa Yesu ni Mwana wa Daudi, Mwana wa Ibrahimu. Kwa hiyo basi anaanzisha mstari wa kuanzia Ibrahimu na kuendelea hadi kwenye mstari wa Yuda. Ndugu ambao wametajwa tu. Huu ni unabii wenye kueleweka. Mstari unaovuja mapokeo na unamtaja mwanamke tangu kwenye aya ya 3-6.

Mathayo 1:3-6 Yuda akamzaa Peresi na Zera kwa Tamari; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu; 4 Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni; 5 Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu; Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu; Obedi akamzaa Yese; 6 Yese akamzaa mfalme Daudi.

 

Wanawake wanaotajwa ni Tamari, Rahabu, Ruthu, na Bathsheba ambaye alikuwa ni mke wa Uria. Maana na umuhimu wa wanawake hawa yanaonyesha somo fulani na maalumu kwenye mlolongo wa uzao huu. Sara hakutajwa. Alikuwa na umuhimu na maana isiyo na mashaka kuliko wote. Fruchtenbaum anaweka pointi za muhimu sana kuhusu wanawake hawa.

Kwanza, wote walikuwa ni Wamataifa. Hivi ndivyo ilivyokuwa dhahiri kwa Tamari, Rahabu na Ruthu. Huenda ilikuwa ni kweli kwa Bathsheba, kwa kuwa mu mume wake wa kwanza, Uria, alikuwa Mhiti. Hapa Mathayo anaongelea kitu fulani na kisha anakiweka wazi baadae: kwamba wakati lengo kuu la kuja kwa Yesu lilikuwa ni kuja kuwaokoa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli, Wamataifa angeweza pia kufaidika na ujio wake. La pili, watatu kati ya wanawake hawa walikuwa na hatia ya dhambi ya uzinifu. Bathsheba alikuwa na hatia ya uzinifu, Rahabu alikuwa kahaba na Tamari alikuwa na tuhuma ya kuolewa na ndugu wa damu. Tena, Mathayo anadokeza tena vitu kwa kiasi kwamba ambavyo alikuja kuainisha baadae kama: kwamba lengo la ujio wa Masihi lilikuwa ni kuwaokoa wenye dhambi...

 

Kuwapatanisha wenye dhambi kwa Mungu ni hatua ya msingi ya kujitoa kwake dhabihu Masihi. Hii ni hatua ya msingi nay a muhimu ya Injili.

 

Ni wale wasioielewa tu maana ya kiroho ya neema iokoayo ya Masihi ndio wanakuwa wametingwa na mambo mengi kwa kujaribu kuthibitisha kwamba wanawake hawa hawakuwa Wamataifa na kwamba hawakuwa wadhambi. Ni muhimu kwamba wadhifa wao ulipewa wajibu wenye lengo la Masihi azaliwe kupitia kwao. Sadaka yake aliyoitoa inatosha. Hii haieleweki kikamilifu. Kwa hiyo muda unapotea kwa kujaribu kuthibitisha kwamba Rahabu alikuwa wa uzao wa Waisraeli wenye asili ya Kikanaani. Pia ni kwamba alikuwa ni mjane kwa mujibu wa maneno ya Sanskrit kwa mlinzi wake wa ndani. Ukweli ulikuwa ni kwamba alikuja akitokea kwenye familia mashuhuri. Watu wake, kwa imani ni kidini ya wakati ule, walikuwa wanafanya ibada za kingono hekaluni na kwa hiyo ilikuwa ni vigumu sana kuepukana nazo, ukiachana na ukweli kwamba alikuwa ananyanyapaliwa sana kwa sababu hii.

 

Muda hautoshi pia kuthibitisha kwamba Ruthu hakuwa mwanamke wa Kimoabi, kutokana na kuingiliana kwake ki Mahusiano ya kindoa na Mmoabi, licha ya jinsi yanavyosema maandiko. Inadaiwa kwamba kwa kweli alikuwa ni wa uzao wa Israeli wa huko Moabi anayedhaniwa kuwa huenda alikuwa wa kabila la Manase, Reubeni au Gadi (Yoshua 1:12-15). Hilo sio la muhimu, kwamba kwa maneno ya Ruthu mwenyewe yanaonyesha kwamba mungu wa watu wake alikuwa ni wa tofauti na yule wa Naomi na kwamba hakuapa kwa Naomi tu peke yake bali pia kwa Mungu wake (Ruthu 1:16).

 

Ukweli wa mambo ulikuwa ni kwamba mstari wa familia ya kifalme ulifunguliwa kwa Wamataifa na kwa wenye dhambi ukianzia kwenye harakati za tangu mwanzoni kabisa za makabila ya Kanaani. Tendo hili lina maana yake kubwa kwa watakatifu.

 

Jambo linguine kubwa kwenye mstari huu wa uzao aliouonyesha Mathayo ni kwamba yeye anachagua kwa umakini anapoutaja mstari wa uzao. Sulemani anatajwa pia kuwa kwenye udugu wa damu unaotokana nay eye. Alilijenga hekalu. Hata hivyo, alibobea pia kwenye ibada za sanamu na mstari wake wa uzao ndipo umeorotheshwa kwa Yekonia aliyekuwa ni mmoja wa wafalme wa mwisho kabla ya kuanza kwa utumwa wa Babeli. Mstari wa uzao wa Yusufu kwa hiyo imewekwa kutoka kwa Yekoania hadi Yusufu. Kwa hiyo, Yusufu ni wa uzao wa Daudi lakini kwa kupitia Yekonia. Jambo hili lina maana sana.

Yeremia 22:24-30 Kama niishivyo mimi, asema Bwana, hata Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, angekuwa pete yenye muhuri katika mkono wangu wa kuume, ningekung'oa wewe hapo; 25 nami nitakutia katika mikono ya watu wale wakutafutao roho yako, na katika mikono yao unaowaogopa, naam, katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya Wakaldayo. 26 Nami nitakutupa nje, wewe na mama yako aliyekuzaa, mwende nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko. 27 Lakini nchi ile ambayo wanatamani kuirudia, hawatairudia kamwe. 28 Je! Mtu huyu, Konia, ni chombo kilichodharauliwa, na kuvunjika? Ni chombo kisichopendeza? Mbona wametupwa, yeye na wazao wake, na kutupwa katika nchi wasiyoijua? 29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana. 30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.

 

Kinia inaundwa kwa kutokana na kuondolewa kwa neno Ye kutoka kwenye neno Yekonia au Mwacheni Yehova (au Jah) atawale. Kuondolwa kwa jina takatifu kunamaanisha kuonyesha kuondoka wa Mungu kutoka kwa Yekonia. Ashirio lake au mkono wa kuume wa Mungu unaonekana kwenye aggai 2:23.

Hagai 2:23 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema Bwana, nami nsiitakufanya kuwa kama pete yenye muhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema Bwana wa majeshi.

 

Zerubabeli aliorodheshwa kwenye Mathayo kuwa ni mwana wa Shealtieli. Hata hivyo tunajua kutokana na 1Nyakati 3:18-19 kwamba alikuwa mwana wa Pediya. Tena Mathayo na pia Ezra 3:2; 5:2 wanasema alikuwa ni mwana wa Shealtieli.

1Nyakati 3:17-19 Na wana wa Yekonia, huyo aliyechukuliwa mateka; mwanawe Shealtieli, 18na Malkiramu, na Pedaya, na Shenazari, na Yekamia, na Hoshama, na Nedabia. 19 Na wana wa Pedaya; Zerubabeli, na Shimei; na wana wa Zerubabeli; Meshulamu na Hanania; na Shelomithi alikuwa umbu lao;

 

Mkanganyiko huu unatatuliwaje? Andko linaonyesha kabisa mahudhui ya tarati.

 

Kumbukumbu la Torati 25:5-6 Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe. 6 Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli.

 

Kazi hii ni ya lazima. Kushindwa kumtimizia majukumu haya (kwa mwanamke mwenye tamaa ya kupenda ngono) ilikuwa ni dhambi ambayo kwayo ilipelekea kuuawa kwa Onani (Mwanzo 38:8-10).

 

Ndipo Zerubabeli alirithi kwenye mstari wa uzao wa Sheltieli kwa kuruhusiwa kihalali kulikowekwa na Pediya aliyekufa baadae. Ndipo Shenaza akafanyika kuwa mwingia nyumba au mlinzi wa Zerubabeli wakati wa kurudi kwao Israeli kama ilivyoandikwa kwenye Ezra 1:8-11; 5:14-16 wakati alipomrudia Sheshibaza.

 

Kamusi ya Strong na nyinginezo zinashikilia kwamba Sheshibaza kuwa ni jina la Kiajemi la Zerubabeli kwa kuwa kuwa na mtu mwingine haiwezekani kwa kuwa kuwa na mtu mwingine haiwezekani, na Zerubbabeli ni kijana sana, anahitaji kulijenga hekalu ili lijengwe tena mahala pake bila kukosewa wakati wa utawala wa Dario II, badala ya kulikosea wakati wa utawala wa Dario I, ambavyo ndivyo wanavyoamini makundi yote, yaani marabi wa Kiyahudi na wahafidhina wa Kikristo kwa sababu zao wenyewe (soma majarida ya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu [013]; na la Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Kina Ezra na Nehemia [250]).

 

Kutokana na unabii uliotolewa kupitia Yeremia, mstari wa uzao ulipunguzwa zaidi. Mungu alitamka kwamba hakuna mtu wa uzao wa Yekonia atakayefanikiwa kuketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme wa Daudi na kutawala tena kutoka Yuda. Hata hivyo, uzao wa Zerubabeli ulikuwa kwenye mstari, ikionyesha kwamba Mungu aliuchagua uzao wake kwa kazi fulani maalumu kama pete ya thamani. Kwa maneno mengine, ni kama mhuri wa Mungu. Hivyo basi Masihi asingeweza kuwa mwana alisia wa Yusufu na kuketi juu ya kiti cha enzi, pasipokuwa na uthibitisho maalumu wa mbingu vinginevyo, Maandiko yangekuwa yametanguka. Kristo angekuwa hana vigezo vya kuketi kwenye kiti cha enzi iwapo kama angekuwa ni mtoto wa kimwili wa Yusufu, na kwa kuwa Yusufu mwenyewe hakuweza kuwa mrithi kabisa, basi asingeweza kiritai cheo hiki kwa njia ya kujitwalia. Mungu anaweka kando na kutengeneza mavunjiko na kuurejesha mstari huo kwa namna nyingine. Mathayo analijua tatizo hili. Na ndiyo maana anaianza Injili kwa mstari unaoonyesha tatizo na kisha anataja tukio la bikira kumzaa mtoto jambo ambalo aliliona wazi kuwa ni kama kulishinda tatizo. Kinachofuatiwa na uzao huu. Mathayo 1:18-25 inaonyesha kwamba ingefanyika tu kwa mimba ya mwanamwali bikira Mariamu au Miriamu (Maria) na kwamba ndiye angemzaa Kristo na kuketi kwenye kiti cha enzi. Tukio hili lina maana yake kwa Wayahudi na kwamba kwa kupitia Masihi ndipo wangeweza kuufikia ufalme wa kiroho na ukuhani w kiroho.

 

Kuna jambo la tatu kwenye mstari wa huu wa uzao wa Zerubabeli ambalo linahitaji kutathimiwa.

 

Zorobabeli alikuwa ni wa kizazi cha 23 kwenye mstari wa wanaume kilichoibuka kutokana na Mfalme (Na. 1). Alikuwa ni mrithi aliyekubalika. Maelezo ya kina ya jamii yake ya mababu na suluhu ya mababa wawili vimeorodheshwa kwa yeye kuwa Shealtieli na Pediya (1Nyakati 3:19) kunafafanuliwa kwenye sharia za Kilawi na ufafanuzi wake hapo juu. Jambo kuhusiana na mstari huu limefafanuliwa pia kwenye jarida la Kutoka Daudi na Matukio ya Misafara wa Kurudi Kutoka Utumwani hadi Nyumba ya Windsor (Na. 67), kwa mujibu wa matukio ya nyakati-zama ua Kiyahudi kwa kutumia mkururo wa matukio ya Dario I. Hesabu sahihi ya nyakati hizi imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu [013].

 

Zorobabeli alikuwa ni mrithi stahiki wa jamii ya kifalme ya Kiyahudi na alikuwa kwenye Msafara wa 3 wa waliorudi kutoka utumwani Babeli mnamo mwaka 545 KK. Alikuwa ni Liwali wa 8 wa Yudea mnamo mwaka 537-536 KK. Alikuwa ni Mfalme wa Yuda mnamo mwaka 515 KK, na alikuwa alishitakiwa na kufungwa mwaka 513 KK na akauawa mwaka 510 KK.

 

Alioa wanawake watatu. Mke wa kwanza alikuwa ni Amytis Binti Mfalme wa Kibabeloni, aliyeitwa kuwa ni mwanamke wa kigeni. Alimzalia mtoto aliyeitwa Shazreza, ambalo ni jina la Kibabeloni. Alikuwa ni mtu aliyetokea kwenye jamii kubwa ya mstari wa mfalme Daudi.

 

Mke wa pili wa Zorobabeli alikuwa Rhoda ambaye alikuwa ni Binti Mfalme wa Kiajemi ambaye baadae aliolewa tena na Mwana Mfalme wa Kiajemi na aliitwa pia aliitwa mwanamke wa kigeni. Alimzalia mtoto aliyeitwa Reza (jina la Liajemi). Alisemekana kuwa ni mjomba wa Dario, mfalme wa Uajemi kwa kupitia mama yake. Ni mstari huu auliotajwa kwenye uzao wa Mariamu kama tutakuba;iana kwamba mstari wa uzao wa Zorobabeli kwamba kwa kweli ulikuwa unapitia kwa Nathani na mwana wa kumkuta au wa kuasiliwa wa Yekonia, aliyeitwa Shealtieli ambaye alikuwa kwa kweli ni mwana wa Neri(a). kitendo cha Kumvika taji Binti Mfalme Tamari kilikuwa ndiyo sababu ya kubadilika kwa mstari huu. Hili ni tukio lingine kwa Binti mfalme Tamari lililotumiwa kubadilisha ufalme. Tutaelezea na kufafanua kwa kina jambo hili baadae hapo chini.

 

La tatu, Zorobabeli alimuoa Esthra, ambaye alikuwa ni binti mfalme wa Kiyahudi. Na kutokana na yeye mstari wa familia iliyopo ya kifalme umetokea.

 

Unabii kuhusu kiti cha enzi na mahali pa Zorobabeli kwenye mchakato unaonekana kuwa ni sehemu ya mchakato wa haki ya ahadi ya uzaliwa wa kwanza ya siku za mwisho.

 

Kumbuka kwamba baba wa Zorobabeli alikuwa ni Shealtieli/Pediya na baba wa Shealtieli kwa kweli hakuwa Yekonia. Alikuwa ni mwana wa kufikia wa Yekonia na alikuwa ni mrithi aliyekubalika au anayestahili (Mathayo 1:12). Alikuwa ni mwana wa mke wa mke wa Mfalme Yehoyakini au Yekonia kwa mke wake wa zamani wa Binti Mfalme Tamari, aliyeitwa Mwana Mfalme Neri(a). Soma pia Luka 3:27. Sasa ukweli huu unatoa mwibuko mwingine wa jambo unaotokana na mstari wa uzao wa Zorobabeli au Zerubabeli ambao kwa kweli ndiyo aliotokea.

 

Tunaona kwamba mstari ulio kwenye injili ya Luka ulikuwa ni wa Daudi kwa kupitia kwa Nathani, na mstari ulio kwenye Mathayo ulikuwa ni wa Daudi kupitia kwa Sulemani. Iwapo kama ufafanuzi huu unakubalika, kw hiyo mstari wa Yekonia na laana iliyotangazwa kwa hii imeshindwa kwenye kile ambacho mstari wa kupitia Zorobabeli kupitia kwa Shealtieli. Hata hivyo, ukweli ni kwamba baba alidaiwa kuwa ni Pedaya kwa mujibu wa sheria za Kilawi, na kizazi kinaenda hadi kwenye mstari wa baba yake. Mstari ule kwa kweli ni wa Nathani kupitia kwa Neri au Neria. Ni sawasawa tu kabisa na kwamba hii ilikuwa ndiyo sababu iliyokuwa imetumiwa kuishinda laana waliyotamkiwa watu wa jamii ya mstari wa Yekonia. Shealtieli anaonekana kuwa ni mlengwa kwenye mjumuisho wa mistari hii. Mistari hii kwa hakika inatuama kwenye kiti cha enzi cha Yuda, ukiishia utumwani, na umefanya vya kutosha kwa karne kadhaa, na kwa hivi karibuni sana kwa makabila kumi.

 

Ukweli mkuu kwa yote haya ni kwamba tunaweza kukioka au ukiibua kizazi hiki kwenye nyumba za kifalme za Israeli hadi kwenye pande za Kaskazini mwa Ujerumani na Uingereza ambao ndiyo makabila ya Kaskazini ya Israeli. Ufalme unabakia ndani ya Israeli hadi sasa hadi atakaporudi Masihi ambaye utakuwa ni haki yake.

 

Mfalme Halali wa Yuda

Kuna umuhimu mkubwa sana kujua kwamba kwenye mstari wa Waliokuwa kwenye Msafara wa kurudi kutoka utumwani (kama lisemavyo jarida la Cox ibid, (Na. 67) hapo juu), kwamba mwaka 12 KK ambao ndiyo miaka ya mwanzoni mwanzoni kabisa ya Kristo aliyotarajiwa kuwa angezaliwa na ambayo kwa kweli ni mwaka wa kutangazwa kwa amri ya kuhesabu watu iliyotolewa na Augustus ambavyo ni hesabu iliyofanyika mara kwa mara kwenye Dola ya Kirumi ulitangulia, hakukuwa na Mtoka kwenye Msafara wa kurudi utumwani aliyetawazwa kwenye kiti cha ufalme wa Yuda. Tangu wakati huu na kuendelea mbele walifukuzwa. Ilikuwa tu baada ya kuzaliwa kwa Mwasihi mwaka 30 BK kwamba alikuwepo mtoka kwenye Msafara wa kurudi utumwani aliyetawazwa kupewa kiti cha enzi cha ufalme wa Yuda. Hivyo basi, Mungu hakuruhusu mfalme bandia awekwe kwenye kiti cha enzi, au astahilishwe na kupendekezwa au kuchaguliwa kuchukua kiti cha enzi Yuda wakati wa mzunguko wote wa mchakato wa kuzaliwa kwa Yesu Kristo ambaye ndiye alikuwa mfalme stahiki wa ufalme wa Yuda.

 

Kuna jambo lingine kuhusu mstari huu wa uzao linaloweka taswira nalo ni kwamba kuna idadi kubwa ya vizazi vilivyotajwa kwenye Mathayo 1:17.

Basi vizazi vyote tangu Ibrahimu hata Daudi ni vizazi kumi na vinne; na tangu Daudi hata ule uhamisho wa Babeli ni vizazi kumi na vinne; na tangu ule uhamisho wa Babeli hata Kristo ni vizazi kumi na vinne.

 

Kujikusanya kwa vizazi hivi kunaonekana kuwa na maana kwenye idadi ya makundi. Kundi la uzao wa Masihi lina maana kubwa sana tangu Adamu. Vizazi saba vya mwanzo tangu Adamu vina maana kwenye Mpango wa Wokovu. Kitendo cha kugawa makundi kwenye injili ya Mathayo ya makundi matatu ya kumi na nne kumi na nne kinaonyesha tu utendaji kazi wa Mungu. Ibrahimu aliitwa na kutengwa mbali na wengine. Vizazi kumi na nne baadae ndipo Daudi mtu wa kawaida tu aliteuliwa na kutengwa mbali na wengine (1Samweli 16:13). Daudi akawaweka pamoja Israeli kama mtawala na kulijenga Heklu kwa kupitia mwanae Sulemani ambaye kwaye, ndpo aliliandaa taifa na raslimali zake. Viazi kumi na nne vilivyofuatia baadae matokeo ya mwisho ya utawala wa kibinadamu na ufalme ulikuwa ni tukio la kwenda utumwani. Vizazi kumi na vinne vilivyofuatia baadae, baada ya taifa kuwa limefanya upya chini ya ukuhani, ndipo itabidi wahukumiwe kipindi cha kuja kwake Msihi na kutawanyishwa kwa Ishara ya Yona (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 13) ibid.). jambo hili halikueleweka.

 

La muhimu zaidi ni kwa,ba kizazi cha 42 kilicho kwenye injili ya Mathayo kuanzia Ibrahimu hadi Kristo kinatajwa kwenye dhana iliyokutikana kwenye ujenzi wa Hekalu. Hekalu lilijengwa kwa mpango wa kiroho wa Yubile. Migawanyo sita iliyogawanywa inafananishwa na neva au mlango unaoonyesha mfano kwamba Masihi aliweka milango mingi kwenye hekalu inayoweza kuingilika vizuri wakati atakaporudi. Kwa kufa kwake alilipasua pazia la Hekalu ili kufungua njia wazi hadi mahali paitwapo naos au Patakatifu pa Patakatifu, ambapo ndipo walipo wateule wake (1Wakorintho 3:16). Njia hii ilifunguliwa yote kabisa tangu kuangamizwa kwa lile Hekalu lililojengwa kwa mikono ya wanadamu (Waebrania 9:8).

 

Vyote viwili, yaani ukuhani na ufalme vilianzishwa na kuhukumiwa vikitakiwa na Masihi. Kwa hiyo Masihi alikuwa ni Masihi wa Haruni na wa Israeli; na alikuwa ni wa namna zote mbili, yaani Masihi-kuhani na Masihi-mfalme. Masihi mmoja mwenye ujio wa mara mbili alikubalika na Israeli, kama tujuavyo kutokana na magombo yaliyovumbuliwa yajulikanalo kama Dead Sea Scrolls (soma kitabu cha G. Vermes cha Gombo za Bahari ya Chumvi (The Dead Sea Scrolls) kwenye lugha ya Kiingereza, re Damascus Rule VII and the fragment from cave [mmeguko kutoka pangoni] IV). Vermes, kama walivyo wengine, anashikilia kuamini kwamba Masihi wa Haruni na Masihi wa Israeli walijulikana kuwa ni mmoja huyo huyo wa majilio tofauti kutokna na imani ya Wayahudi wa karne ya kwanza.

 

Jibu la matatizo haya yaliyoibuka kutoka kwenye mstari wa uzao ulio kwenye injili ya Mathayo linajibiwa na yeye kwenye sura ya 1:18. Maibu makuu na ya zaidi kwenye maandiko haya ni kwenye injili ya Luka. Kwa hiyo, yote mawili yanapaswa yasomwe kwa muunganiko au kwa kuhusianisha.

 

Hatua nyingine na ya muhimu iliyofanywa na Arnold Fruchtenbaum kuhusu mstari wa uzao wa Masihi, ambao pia una maana pana zaidi ni kwamba mapokeo ya Kiyahudi ya wakati ule. Anasema hivi kuhusu maelezo ya Luka:

Mbali na Mathayo, Luka kufuatia kikamilifu mwelekeo na mapokeo yaliyopo hakuruka au kuacha majina na wala hakuwataja wanawake. Hata hivyo, kama kwa mujibu wa mapokeo ya Kiyahudi mtu hakuweza kulitaja jina la mwanamke, bali alipenda kuonyesha mstari wake, ni kwa jinsi gani aliweza kufanya hivyo? Angelitumia jina la mume wake. (Karibu Agano lote la Kale linaanza kwa tendo hili la kwenye Ezra 2:61 na Nehemia 7:63).

 

Hiyo ingeibua swali la pili la kwamba: Kama mtufulani alisoma mstari wa uzao, angewezaje basi iwapo kama uzao huo ulikuwa ni ule wa mume wake au ni ule wa mwanamke, na iwapo kama kwa sababu hiyo jina la mume lingetumikaje? Jibu lake sio gumu, tatizo linatokana na lugha ya Kiingereza.

 

Kwa Kiingereza siyo grama nzuri kutumia kiamhishi halisi (the) kabla ya jina halisi (‘the’ Matthew, ‘the’ Miriam); haya hivyo, inaruhusiwa sana kwenye grama ya Kiyunani. Kwenye maandiko ya Kiyunani ya uzao ulioandikwa kwenye injili ya Luka, kile jina moja lililotajwa lina kiambishi cha Kiyunani cha ‘the’ pamoja na nyingine isiyo ya kawaida: jina la Yusufu (Luka 3:23). Mtu anayesoma maandiko yenyewe ya asili anaweza kuelewa kwa viambishi vingine vinavykosekana kwenye jina la Yusufu kwamba huu haukuwa mstari halisi wa uzao wa Yusufu bali ni mke wake, yaani wa Mariamu.

 

Zaidi sana, ingawa tafsiri nyingi za Luka 3:23 zinasomeka kwamba: “...akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli, ...”, kwa sababu ya kiambishi muhimu kinachokosekana kwenye Kiyunani cha kabla ya jina la Yusufu, ni aya hiyohiyo ingeweza kutafsiriwa kama: “Na akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,...” (msisitizo umewekwa).

 

Kwa naneno mengine ni kwamba ingawa Yehoshua (Yeshua, Yoshua au Yesu) alitakiwa kuwa mwana wa Yusufu, lakini kwa kweli alikuwa ni wa uzao wa Eli ambaye alikuwa ni Baba wa Mariamu. Tafsiri ya Jerusalem Talmud iliuchukulia mstari huu wa uzao kuwa ni wa Mariamu na sio wa Yusufu. Inamtaja Mariamu kuwa ni kama binti wa Eli kwenye Hagigah 2:4.

 

Kutumika kwa makala maalumu kwenye uandishi wa Kiyunani pia unauhusiano wake kunapowekwa tofauti kati ya Masihi na Mungu, kwa mfano kwenye Yohana 1:1,18; 1Yohana 5:20. Hili limeonekana kutimilika kwa kipindi zama kimoja hadi kingine na dini kwa kutokubaliana na kile kinachoitwa uhafidhina (mfano ni maandiko ya Socinians; soma kitabu cha ufafanuzi cha Heydock hadi kwenye marudio ya chapisho ya mwaka 1851 ya Kikatoliki au tafsiri iitwayo Douay-Reims Bible).

 

Luka anaonyesha kumuweka Kristo kwenye zama za nyuma sana hadi Adamu ambapo ni kuonyesha mchakato wa uzao wa mwanamke tangu Adamu. Andiko hili linauonyesha mstari wa uzao wa Daudi pamoja na Nathani ambao ni muhimu kwa kutimiliza unabii ulio kwenye Zekaria. La muhimu sana ni kwamba mbali na mstari wa uzao wa Yekonia ambao ulikuwa umeondolewa, miongoni mwa mambo mengine ni fanya njia ya utawala wa Kuhani Mkuu. Kwa hiyo, Yehoshua au Yoshua alikuwa ni wa uzao wa Daudi kutoka kwa mama yake. Kwa hiyo, kuzaliwa na mwnamwali bikira mbali kunaendelezwa kwanza na kisha uzao untajwa hapa kwenye Luka. Na kwa hiyo inaanzisha sharti la kwanza kwa udugu ambao ni wa mstari wa uzao wa Daudi mbali na ule wa Yekonia.

 

Anaanzisha sharti la pili la kufanyika kuwa wa mstari wa Nathan na wa familia ya Lawi kwa kupitia Shimei kwa kando na mlolongo wa uhusiano wa familia ya Miriam hadi kwa Elisabeth mke wa Zakaria, Kuhani Mkuu wa Zamu ya Abiya (au Abia), ambayo alikuwa ni wa zamu ya nane ya Kuhani wa Hekaluni (soma 1Nyakati 24:10; Nehemia 12:17). Zamu au migawanyo ishirini na nne iliundwa baada ya kurudi kutoka kwenye migawanyo ya njia ya kura, kwa majina yenyewe halisia (soma Comp. Bible fn. na App. 179 III).

 

Mke wa Zakaria alikuwa Elisabeth (aliyeitwa jina lake kutokana na jina la mke wa Haruni Elisheba (Kutoka 6:23) na akamvuvia Elizabeth kwenye LXX). Alikuwa ni binti wa Haruni na kwa hiyo alikuwa ni Mlawi (Luka 1:5). Alikuwa ni mama yake Yohana Mbatizaji kwa minajiri ya kimungu. Kwa hiyo Yohana alichaguliwa. Mariamu (Maria) alikuwa ni wa kutoka familia ya Elizabeth (Luka 1:36). Kwa hiyo ni lazima Mariamu atakuwa ni wa mstari wa kidamu wa kabila la Lawi pamoja na kuwa ni wa Nyumba ya Daudi.

 

Tunadhania tu kiunasibu kwenye mstari wa ukoo wa Lawi kwa kupitia Shimei, hata hivyo inaweza kudhaniwa au kuchukuliwa, kwa kuwa Maandiko hayawezi kutanguka. Kuonyeshwa kwa mstari wa ukoo wa Walawi kunatosha. Uvuvio wa kimungu wa Zekaria na Elisabeth na ndipo jina la Yohana linatupeleka kwenye hatua nyingine inayofuatia.

 

Walikuwepo wengine kwenye Nyumba ya Daudi na sio wa mstari wa Yekonia. Hivyo jambo lenyewe ni lazima liwe ni la kuruhusiwa na mbingu ambapo linaweka kigezo cha sharti la tatu kwa kufanyika mfalme. Luka anaendelea kuweka vigezo cha kuchaguliwa na mbingu kwenye Luka 1:30-33.

Luka 1:30-33 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. 31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. 32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. 33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

 

Kwa hiyo ndipo Bwana Mungu alimpa kiti cha enzi cha baba yake Daudi. Alitimiliza vigezo kwa kupangiwa au kuruhusiwa na Mungu.

 

Alikuwa ni wa uzao wa mwanamke kama ilivyikuwa imetabiriwa kwenye kitabu cha Mwanzo. Mathayo inaonyesha ni kwa nini hakuwa mfalme anayetokana na uzao wa Yusufu bali ni wa kuzaliwa tu na mwanamwali na ni mpango wa kimungu. Luka anaonyesha kwa jinsi ipi alitimiliza unabii mwingine na hakueleweka vizuri na ama marabi wa Kiyahudi au Wafafidhina wa Ukristo mkongwe. Malengo ya marabi kwenye Umasihi wake kwa maana ya kwamba ni lazima iwe ni kwa kupitia mstari wa baba yake wawe waongo kwa minajiri ya unabii na kigezo cha kuwa mwana wa Mungu. Elohim wa Israeli asingeweza kuchukua hali ya ubinadamu ma maana ya kihalisia. Alifanyika mwanadamu kwa kuelekezwa na elohim wake ambaye ndiye El Elyon, Mungu Aliye Juu Sana. Kigezo hiki kilitabiriwa na nabii Isaya ambaye alisema:

Isaya 7:14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

 

Sio kwamba kuitwa kwake Mungu pamoja nasi kunaweza kufikiwa tu iwapo kama El aliyetumwa hapo mwanzoni alikuwa elohim na kwa kweli ni elohim wa Israeli aliyetiwa mafuta kuwa elohim na elohim wake kama inavyoonekana kwenye Zaburi 45:6-7. Alipata haiba yake ya uwanadamu kikamilifu sana kutoka kwa mama yake. Kwa hiyo, mapokeo ya taifa la Kiyahudi na utambulisho wa kikabila vililetwa na kiumbe huyu ili kwamba aweze kufanya shughuli za kikuhani baada ya Melkisedeki na kisha afanyike kuwa kichwa au kiongozi kwa utaratibu wa wafalme na makuhani waliochaguliwa mbali na mstari ila ilifanywa kwa mkabila yote kama tunavyoona kwenye Ufunuo 7:3-8.

 

Yeye ni mwana wa Daudi na mwana wa Ibrahimu kutokana na Mathayo 1:1. Luka 3:38 kunakomtaja yeye kuwa ni mwana wa Adamu na mwana wa Mungu. Kwa hiyo anajipatia mambo mengi zaidi na maradufu pia kwenye injili. Akiwa kama mwana wa Daudi, yeye ni Mfalme wa Yuda yote. Na akiwa kama mwana wa Ibwahimu, yeye ni Mfalme wa Israeli kama mrithi wa ahadi zilizotolewa na kwa kupitia Yusufu. Yeye pia ni kiongozi au kichwa cha mataifa mengine ya Ibrahimu. Akiwa kama mwana wa Adamu yeye ni mwanadamu na hivyo anastahili kuwaongoza wanadamu kwenye wokovu kwa kupitia kifo chake. Akiwa kama mwana wa Mungu anafika kimo cha wadhifa wa elohim ambacho alikichilia wakati alipokuja kuzaliwa kimwili, na kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu akiwa kama mwana wa Mungu mwenye nguvu na uweza (Warumi 1:4). Anastahili kuwa Nyota ya Asubuhi na atashiriki utawala ule pamoja na watu wote wa nyumbani mwake (Ufunuo 2:27-28; 22:16; sawa na Zekaria 12:8) kama wanavyoshiriki asili na  tabia za Mungu kama anavyofanya (2Petro 1:4). Tafsiri ya The Peshitta inasema:

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu. 28 Nami nitampa ile nyota ya asubuhi.

 

Masihi alikuwa mtii hadi kufa na kwa hiyo anatakiwa pia awe mtiifu na atatupa utawala wa Nyota wa Asubuhi ambaye ni Mwana wa Mungu, akiwa kama elohim kama Malaika wa Yahova aktuongoza. (Zekaria 12:8).

q